3.3 Uchunguzi wa shinikizo la juu la damu baada ya kuzaa

Shinikizo la diastoli la damu hupimwa wakati moyo umepumzika katikati ya mipigo ya moyo.

Ishara bainifu ya Shinikizo la juu la damu ya ujauzito ni Shinikizo la juu la damu, kwa kawaida shinikizo la juu ya diastoli ya zaidi milimita90 ya zebaki. Ulijifunza jinsi ya kupima shinikizo la damu ya mama katika Moduli ya Utunzaji katika ujauzito, Kipindi cha 9, na kuhusu matatizo ya damu ya ujauzito katika Kipindi cha 19. Hapa tutashughulika na Shinikizo la juu la damu inayoanza au kurudi wakati wa puperiamu. Ili kuchunguza haya, uliza mama kuhusu dalili zifuatazo:

  • Maumivu ya kichwa, pamoja na au bila matatizo ya kuona (kutoona vizuri), na wakati mwingine kichefuchefu na kutapika.
  • Mtukutiko kali zaidi (eklampsia). Hakikisha kwamba unajua istilahi ya mtukutiko inayotumika pale. Inaweza kuelezwa kama isiyo kuwa ya kawaida na isiyoweza kuzuilika zilizoambatana, kwa mikono na miguu, na au bila kupoteza fahamu.
  • Kuvimba kwa (edema) mikono na miguu, au hata uso.
  • Maumivu makali katika sehemu ya juu ya fumbatio.

Pima mkojo kwa kutumia kijiti cha kutumbukiza (kama ulivyofunzwa katika Kipindi cha 9 katika Moduli ya Utunzaji katika ujauzito). Mkojo ukipimwa na kijiti cha kutumbukiza kubaini kuwepo kwa protini, mama aliye na Shinikizo la juu la damu anaweza kuonyesha kuwepo kwa protini. Kuwepo kwa protini huonyeshwa juu ya kijiti cha kutumbukiza kutoka +1 hadi +3 na zaidi. Iwapo mojawapo ya uchunguzi uliyotajwa hapo awali uko, shuku Shinikizo la juu la damu iliyosababishwa na ujauzito. Rufaa mama haraka kwenye kituo cha afya kilicho karibu. Kumbuka kwamba shinikizo la damu baada ya kuzaa inaweza kuwa kwa mama yeyote, hata kwa yule ambaye alikuwa na shinikizo la damu la kawaida na hakuwa na dalili yoyote wakati wa ujauzito, leba, na kuzaa.

3.2.4 Maambukizi kwa kidonda

3.4 Mvilio ndani ya mshipa wa damu