3.4 Mvilio ndani ya mshipa wa damu

Mvilio ndani ya mshipa wa damu- damu huganda, karibu kila mara katika moja ya mishipa ya ndani ya miguuni - ni tatizo nadra wakati wa puperiamu. Hata hivyo, wakati hutokea, inaweza kusababisha kifo kwa haraka kama ganda la damu litatoka kwa mshipa ya mguu na kuelekea kwa moyo, mapafu, au ubongo, na kuzuia damu muhimu kwa mshipa ya damu.

Uwezekano wa ukuaji wa mvilio ndani ya mshipa wa damu ni kawaida sana wakati wa ujauzito kuliko katika hali isiyo ya ujauzito, na uongezeka zaidi wakati wa puperiamu. Sababu hasa za damu kuganda katika mishipa ya ndani miguuni (mvilio) haijulikani. Hata hivyo, hatari huwa kubwa zaidi wakati mama anakaa muda mwingi kitandani na hafanyi chochote kwa siku kadhaa baada ya kuzaa. Katika sehemu nyingi za Afrika, desturi za nyumbani ni kuwa kina mama, baada ya kuzaa, hawapaswi kujishughulisha na chochote ila tu kukaa kitandani na kutembea tu kwenda chooni. Hivyo ni muhimu utambue dalili na ishara za mvilio ndani ya mshipa wa damu, tekeleza utambuzi na kurufaa mama hospitalini haraka iwezekanavyo. Kisanduku 3.2 linaonyesha dalili na ishara za kawaida za mvilio ndani ya mshipa wa damu.

Kisanduku 3.2 Dalili na ishara za mvilio ndani ya mshipa wa damu

  • Maumivu katika mguu mmoja tu: kawaida hutokea kwa ghafla, ikiwa na uchungu inayoendelea na aina ya maumivu.
  • Uchungu unapogusa: eneo hilo ni uchungu unapogusa mahali hapo.
  • Uvimbe: mguu ulioathirika huwa mkubwa na tofauti kubwa zaidi wa sentimita 2 wa mduara ikilinganishwa na mguu huo mwingine (wenye afya). Uvimbe unaweza kuwa kwa kafu au paja.
  • Ukamba unayohisika: unaweza kuhisi muundo-kama wa kamba ndani ya mguu uliovimba.
  • Mguu kubadilika rangi: mguu ulioathirika unaonekana kuwa nyekundu kidogo.
  • Maumivu kwenye kafu: anahisi uchungu wakati unajaribu kunyorosha kiungo cha kifundo cha mguu

3.3 Uchunguzi wa shinikizo la juu la damu baada ya kuzaa

3.5 Matatizo ya Akilini baada ya kuzaa