Muhtasari wa Kipindi cha 3

Katika Kipindi cha 3, Umejifunza kuwa:

  1. Ingawa wakati muhimu zaidi wa kuvuja damu baada ya kuzaa ni katika kipindi cha tatu na nne cha leba, unapaswa kuendelea kuwa macho wakati wa puperiamu na kumshauri mama kuripoti utokaji wa damu yoyote kutoka ukeni.
  2. Sababu za kawaida za kuvuja damu baada ya kuzaa ni endometiritisi, mikazo duni, plasenta iliyobaka kwa uterasi, na kutoka kwa ngozi kavu katika makao ya plasenta.
  3. Kiasi chochote cha damu kutoka ukeni baada ya saa 24 ya kuzaa inafaa kuchukuliwa kama tatizo kuu na lazima mama apewe rufaa.
  4. Aina kuu za maambukizi baada ya kuzaa ni endometiritisi, mastitisi, maambukizi kwa mfumo wa mkojo, na kwa kidonda, ambazo zote kwa kawida uambatana na joto jingi mwilini.
  5. Hatari zinazochangia endometiritisis baada ya kuzaa ni leba ya muda mrefu, Kupasuka kwa Tando kabla ya Wakati inayochukuwa muda mrefu, uchunguzi wa ukeni kila mara, maambukizi kwa njia ya uzazi sehemu ya chini kabla ya ujauzito, plasenta iliyobaki kwa uterasi, uzaaji uliyo na matatizo ikiwa ni pamoja na upasuaji au kwa kutumia koleo.
  6. Mama ambaye amepata mastitisi baada ya kuzaa, anahimizwa kunyonyesha.
  7. Shinikizo la juu la damu baada ya kuzaa inayohusishwa na Shinikizo la juu la damu, odema, matatizo ya kuona, na mtukutiko (eklampsia), zinaweza kutokea kwa mama ambaye alikuwa na shinikizo la damu la kawaida na bila dalili wakati wa ujauzito, leba, na kuzaa.
  8. Mvilio ndani ya mshipa wa damu inahusishwa na maumivu na kuvimba kwa mguu, na kawaida zaidi hutokea katika kina mama ambao hukaa kitandani kwa siku kadhaa baada ya kuzaa.
  9. Baadhi ya kina mama wanaweza kupata matatizo ya kiafya akilini, ya kawaida na ni ya muda mfupi, ni kununa baada ya kuzaa ambayo si kali. Baadhi ya kina mama wanaweza kupata matatizo makali ya masumbuko, ambayo yanahitaji huduma na matibabu katika kituo cha afya cha ngazi ya juu.

3.5.1 Kununa na masumbuko baada ya kuzaa

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 3