Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 3

Kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki, unaweza kutathmini mafanikio uliyopata katika Malengo ya somo kwa jibu maswali yafuatayo. Andika majibu yako katika shajara na uyajadili na Mkufunzi wako katika Mkutano ujao wa somo. Unaweza kulingasha majibu yako na nakala juu ya Maswali ya Kujitathmini mwisho wa Moduli hii.

Swali la Kujitathmini 3.1 (yanatathmini Malengo ya Somo 3.1, 3.2 na 3.5)

Unajadiliana na mmoja wa mhudumu wa afya mwenzawako kuhusu matatizo ambayo yanaweza kutokea wakati wa kipindi cha puperiamu. Ameanza tu mafunzo yake ya huduma ya afya na anataka kujua kuhusu maneno yafuatayo na dalili zao kuu. Utamwelezea nini kuhusu kila moja ya yafuatayo?

  • a.Kuchelewa kutokwa na damu baada ya kuzaa
  • b.Sepsisi baada ya kuzaa na joto njingi mwilini
  • c.Mastitisi
  • d.Shinikizo la juu la damu baada ya kuzaa
  • e.Masumbuko baada ya kuzaa

Answer

  • a.Kuchelewa kutokwa na damu, baada ya kuzaa ni uvujaji wa damu nyingi ukeni katika wiki ya kwanza na hadi wiki sita baada ya kuzaa. Kutokwa na damu baada ya kuzaa inaweza kuwa tishio kwa maisha na lazima mama apewe rufaa haraka. Visababishi vya kawaida ni pamoja na maambukizi (endometiritisi) ya ukuta wa ndani ya uterasi, mikazo duni ya uterasi, kutoka kwa ngozi kavu katika makao ya plasenta, au sehemu ya plasenta kubaki kwenye uterasi. Kisababishi cha hali hii kwa nafasi ndogo ni ujauzito isiyo kuwa ya kawaida.
  • b.Sepsisi baada ya kuzaa ni maambukizi ya bakteria kwa mfumo wa uzazi yaliyo kawaida sana baada ya kuzaa. Kawaida inaweza kuzuiwa kwa usafi wakati wa kuzaa. Joto jingi mwilini inaonyesha uwezekano wa sepsisi, lakini inaweza pia kuwa ni kutokana na maambukizi kwa mfumo wa mkojo au kidonda, VVU, malaria, homa ya matumbo, pepopunda, meningitisi, nimonia, na kadhalika.
  • c.Titi nyekundu lililo na maumivu huashiria mastitisi, inflamesheni kwa titi kutokana na maambukizi ya bakteria. Kina mama wanaonyonyesha wako katika hatari kubwa ya mastitisi baada ya kuzaa ikiwa mtoto hanyonyi vizuri na matiti hayaishi maziwa yote. Jipu ni hatari nyingine kutokana na maambukizi kwa titi, ambayo hutokea wakati usaha hukusanyika katika tishu iliyoambukizwa.
  • d.Shinikizo la juu la damu baada ya kuzaa ni shinikizo la juu la damu katika Utunzaji baada ya kuzaa. Dalili bainifu ni maumivu makali ya kichwa, mtukutiko (eklampsia), kufura, maumivu makali ya tumbo, na protini katika mkojo. Ni tisho kwa maisha na lazima mama apewe rufaa mara moja.
  • e.Masumbuko baada ya kuzaa ni kali kuliko kununa baada ya kuzaa. 'Kununa' ni hisia kali za wasiwasi na huzuni, au kuchanganyikiwa kwa akina mama wengi huwa nayo baada ya kuzaa na ambayo kwa kawaida huisha. Kina mama wanaopata masumbuko baada ya kuzaa (huzuni unayoendelea na sununu iliochini na motisha kidogo) lazima wapewe rufaa.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.2 (linatathmini Lengo la Somo 3.3)

Kamilisha mapengo yaliyowazi katika Jedwali 3.1, inayorejelea matatizo katika puperiamu.

Jedwali 3.1 Matatizo ya kawaida wakati wa puperiamu
DaliliIsharaUtambuzi unaoweza kuwepoHatua
Kutokwa na damu siku saba baada ya kuzaa
Maambukizi kwa mfumo wa mkojoMshawishi mama anywe kiowevu na umpatie rufaa
Uchungu kwa titi na joto jingi mwiliniTiti chungu inapogushwa, moto, na nyekundu
Uchungu kwa msambaKukatika kwa msamba na kutokwa na mchozo wa rangi ya manjano na uchungu ukigusa

Answer

Jedwali 3.1 lililokamilishwa linaonekana kama ifuatavyo:

Jedwali 3.1 Matatizo ya kawaida wakati wa puperiamu.
DaliliIsharaUtambuzi unaoweza kuwepoHatua
Kutokwa na damu siku saba baada ya kuzaa Uterusi ikiwa katikati ya kitovu na pelvisiEndometiritisisiAnza kumpatia kiowevu kwa mshipa
Kukojoa mara nyingi na kwa harakaUchungu kwenye pelvisi juu ya kibofuMaambukizi kwa mfumo wa mkojoMshawishi mama anywe kiowevu na umpatie rufaa
Uchungu kwa titi na joto njingi mwiliniTiti chungu linapoguswa, moto, na nyekunduMastitisi, labda jipu kwa titiMpatie dawa ya kupunguza uchungu na umpatie rufaa
Uchungu kwa msambaKukatika kwa msamba na kutokwa na mchozo wa rangi ya manjano na uchungu ukigushaMaambukizi kwa kidondaOsha na majimoto yaliyo na chumvi, finya usaha, mpatie, paracetamol ilikudhibiti uchungu, na labda umpatie rufaa ili apate antibiotiki

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.3 (linatathmini Lengo la Somo 3.4)

Umemtembelea mama aitwaye Lakesh ambaye alizaa siku saba zilizopita. Mara ya mwisho ulimwona alikuwa amelala kitandani. Wakati huu anaamka kukusalimia na unamwona kwamba anatembea kwa shinda. Unamuuliza kama ameumia. Anasema ana uchungu wa ghafla katika mmoja wa miguu wake. Unaweza kuthani ni nini na ungefanya nini kuhusu jambo hilo?

Answer

Unapaswa kukumbuka mara moja kwamba hatari ya mvilio ndani ya mshipa wa damu ni kubwa zaidi kama mama analala sana kwa muda mrefu baada ya kuzaa, kama vile Lakesh amekuwa akifanya. Ungechunguza kwa haraka kama ishara yoyote au zote za mvilio ndani ya mshipa wa damu kama ilivyowekwa katika Jedwali 3.2. Iwapo ishara zinakuelekeza kuwa Lakesh ana mvilio ndani ya mshipa wa damu, unafaa kumapatia rufaa kwa kituo cha afya cha ngazi ya juu haraka iwezekanavyo.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.4 (linatathmini Lengo la Somo 3.5)

Mama mwingine aitwaye Almaz yuko katika wiki ya kwanza baada ya kuzaa; anajihisi kila mara mwenye hatia na kujidharau, analia kwa urahisi na anahisi mchovu, wasiwasi, na kukasirika. Ni nini kinaweza kuwa kinamwathiri? Ni dalili gani hatia unaweza kumliza, ili kuthibitisha utambuzi wako?

Answer

Utambuzi unaoweza kuwa kwa hali ya Almaz ni masumbuko baada ya kuzaa. Ili kuthibitisha utambuzi wako, mwulize kuhusu dalili zifuatazo:

  • Kupungua kwa hamu ya chochote au furaha
  • Matatizo ya usingizi, kulala sana, au kidogo sana
  • Upungufu wa uwezo wa kufikiria au kumakinika kwa jambo
  • Ukosefu wa hamu ya kula

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 3