Malengo ya Somo la Kipindi cha 5

Baada ya Kipindi hiki, unafaa kuwa na uwezo wa:

5.1 Kufafanua na kutumia kwa ufasaha maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito.(Maswali ya Kujitathmini 5.1 na 5.2)

5.2 Kuelezea vipimo vya mwili unavyopaswa kufanya kwa mama aliyezaa baada ya kuzalisha, na katika ziara inayofuatia baadaye, ili kuhakikisha kwamba anapata nafuu vizuri. (Swali la Kujitathmini 5.2)

5.3 Kueleza jinsi utamshauri mama kuhusu lishe bora katika kipindi baada ya kuzaa na ni virutubishi vidogo gani za nyongeza ungempa. (Swali la Kujitathmini 5.2)

5.4 Kuelezea aina za usaidizi utakazompa mama baada ya kuzaa ambayo ungemshawishi mpenzi wake na familia yake kumpa, ikiwa ni pamoja na kutafuta huduma ya mara moja iwapo watagundua kuwepo kwa dalili za hatari. (Swali la Kujitathmini 5.2)

Kipindi cha 5 Utaratibu wa Kumhudumia Mama baada ya kuzaa

5.1 Kiini cha utaratibu wa huduma kwa mama baada ya kuzaa