5.1.2 Chunguza kama uterasi yake ina mikazo ya kawaida

Gusa (hisi) fumbatio lake kupima mikazo ya uterasi ili kuhakikisha kwamba iko imara. Mara tu baada ya kuzaa, unapaswa kuwa na uwezo wa kuhisi mikazo karibu na kitovu cha mama, na kuteremka chini katika pelvisi yake kwa mwendo wa kasi zaidi kwa wiki mbili zijazo. Chunguza uterasi yake kila baada ya dakika 15 kwa ya masaa mawili ya kwanza baada ya kuzaa na kila dakika 30 kwa saa ya tatu. Ikiwezekana, chunguza kila saa kwa saa tatu zifuatazo. Iwapo uterasi iko ngumu, iwache wakati wa vipimo. Ikiwa utahisi ikiwa laini, sugua fumbatio juu ya uterasi ili uisaidie iwe na mikazo. Mfunze mama kujifanyia hivi (Mchoro 5.1).

Mchoro 5.1 Uterasi inaweza kusaidiwa kupata mikazo baada ya mama kuzaa kwa kusugua fumbatio.

Dawa ulizompa mama (kwa mfano, misoprostol au oxytocin) kusaidia kutoa plasenta na kuzuia kuvuja damu pia itasaidia uterasi kupata mikazo. Kwa hivyo hunyonyesha mtoto wake. Mama pia anaweza kuwa na haja ya kukojoa ikiwa kibofu chake cha mkojo kimejaa, kinachosaidia uterasi kujikaza vizuri. Chunguza mikazo ya uterasi katika ziara zote baada ya kipindi cha kuzalisha.

5.1.1 Chunguza ishara muhimu kwa mama

5.1.3 Safisha tumbo ya mama, viungo vya uzazi na miguu