5.1.3 Safisha tumbo ya mama, viungo vya uzazi na miguu

Mchoro 5.2 Kuosha eneo la viungo vya uzazi vya mama ni mojawapo ya huduma ya kimsingi baada ya kipindi cha kuzaa katika ziara ya kwanza.

Msaidie mama kujisafisha baada ya kuzaa. Badilisha matandiko yoyote yale chafu na usafishe damu iliyo mwilini mwake. Nawa mikono kwanza na uvae glavu kila mara kabla ya kugusa viungo vya uzazi vya mama, kama ulivyofanya kabla kuzalisha. Hii itamlinda kutokana na bakteria yoyote ambayo inaweza kuwa kwa mikono yako. Safisha viungo vya uzazi vyake kwa utaratibu, kwa kutumia sabuni na maji safi sana na kitambaa safi (Mchoro 5.2). Usitumie kemikali ya kuua viini vya maradhi yoyote ambayo inaweza kuwasha tishu zake zilizonyororo. Osha kuelekea chini, mbali na uke. Kuwa mwangalifu ili usipeleke chochote kutoka mkundu kuelekea ukeni. Hata kipande kidogo cha kinyesi kisichoonekana kinaweza kusababisha maambukizi.

5.1.2 Chunguza kama uterasi yake ina mikazo ya kawaida

5.1.4 Chunguza uvujaji wa damu nyingi (hemoreji)