5.1.5 Chunguza viungo vya uzazi vya mama iwapo kuna miraruko na matatizo mengine

Mchoro 5.3 Fungua vulva kwa utaratibu kuchunguza viungo vya uzazi kwa ishara za jeraha.

Tumia mkono ulio na glavu kwa utaratibu kuchunguza viungo vya uzazi vya mama (Mchoro 5.3) kwa miraruko, vibonge vya damu, au hematoma (kutokwa na damu ndani ya ngozi). Ikiwa mwanamke ana mraruko unaohitaji kushonwa, weka shinikizo juu yake kwa dakika 10 kwa kutumia kitambaa safi au pedi na kumrufaa kwa kituo cha afya. Ikiwa mraruko ni mdogo, pengine unaweza kupona bila kushonwa, bora tu iwe imetunzwa kwa safi ili kuzuia maambukizi katika jeraha.

Mweleze apumzike iwezekanavyo na umwambie kuwa hapaswi kupanda juu au kushuka milima yaliyowima. Mtu mwingine anapaswa kufanya kazi za kifamilia za kupika na kusafisha kwa siku chache. Ili apate nafuu haraka, anapaswa pia kula vyakula vingi vyenyewe afya, kuweka sehemu ya viungo vya uzazi viwe safi (kuosha na maji baada ya kutumia choo) na kufunika kwa kitambaa au pedi safi.

Kuvuja damu ndani ya ngozi (hematoma) au maumivu ukeni

Wakati mwingine uterasi hukazika na kuwa ngumu na utokaji wa damu huwa ni kiasi, Ilhali mama bado anahisi kizunguzungu na mdhaifu. Iwapo hii itatokea, anaweza kuwa anatokwa na damu chini ya ngozi ukeni mwake ambapo huitwa hematoma (Kielelezo 5.4). Ngozi katika eneo hili mara nyingi huvimba, huwa na rangi ya utusitusi, nyepesi kwa kudhurika, na nyororo.

Mchoro 5.4 Hematoma ni mkusanyiko wa damu ndani ya ngozi katika eneo la viungo vya uzazi vilivyo na uchungu.

Seviksi iliyochomoza

Mchoro 5.5 Seviksi iliyochomoza inaweza kuonekana kwa ufunguzi wa uke.

Chunguza kama seviksi imechomoza (imeshuka chini kwa ufunguzi wa uke; Mchoro 5.5). Tatizo hili si hatari, na seviksi kwa kawaida hurudi ndani baada ya siku chache. Msaidie mama kuinua nyonga ili iwe juu kuliko kichwa chake. Mwambie afanye mazoezi ya kukaza misuli ya uke na kuta za pelvisi angalau mara nne kwa siku.

Ikiwa seviksi itabaki katika ufunguzi wa uke zaidi ya wiki mbili, anapaswa kupewa rufaa. Seviksi ambayo itakaa ikiwa imechomoza inaweza kutatiza iwapo mama atapata mtoto mwingine

5.1.4 Chunguza uvujaji wa damu nyingi (hemoreji)

5.1.6 Msaidie mama kukojoa