5.2.3 Kuzuia upungufu wa iodini

Mchoro 5.8 Tezi ni uvimbe ulio mbele ya shingo, unaosababishwa na upanuzi wa glandi ya thiroidi.

Kuongeza madini ya iodini kwa chumvi huitwa iodination na inapendekezwa utumie chumvi iliyo na iodini kwa upishi katika kipindi baada ya kuzaa, hasa katika maeneo ya nchi ambazo tezi ni ya kawaida kama matokeo ya madini ya iodini kidogo sana katika mlo (Mchoro 5.8). Uongezaji wa madini ya iodini kwa chumvi imeonekana kuwa njia yenye ufanisi mno ya kuzuia upungufu wa iodini. Kutumia mafuta yenye iodini kwa njia ya kunywa au kudungwa sindano inaweza kutumika kama hatua ya muda mfupi katika maeneo endemiki ambapo ni vigumu kupatikana kwa chumvi iliyo na iodini. Mshawishi mama atumie chumvi iliyo na iodini kila siku wakati wa kipindi baada ya kuzaa, kama inapatikana. Hata hivyo, kama tezi inapatikana hapo, mama anaweza kupewa dosi ya mafuta iliyo na iodini baada tu ya kuzaa.

5.2.2 Ushauri juu ya lishe baada ya kuzaa

5.2.4 Kuzuia upungufu wa vitamini A