6.1 Hatua za kwanza kabla ya kumchunguza mtoto mchanga

Kabla ya kuanza kumchunguza mtoto mchanga, vua virembesho kama vile pete, bangili au mapambo yoyote mengine, kisha unawe mikono vyema kwa maji safi na sabuni kwa angalau dakika 2. Kunawa mikono ni mojawapo ya hatua muhimu zaidi unayoweza kuchukua ili kuzuia maambukizi. Hakikisha kuwa unabeba sabuni na taulo yako mwenyewe katika kila ziara, na ufuate maagizo yaliopeanwa kwenye Mchoro 6.1.

Kisanduku 6.1 Jinsi ya kunawa mikono vyema kabla ya kufanya uchunguzi wa baada ya kuzaa.

Pia unafaa kumwonyesha mama jinsi ya kunawa mikono yake vyema, na umkumbushe kunawa mikono:

  • Kabla ya kunyonyesha
  • Kabla ya kumvisha au kumvua mtoto nguo.
  • Kabla ya kumsafisha au kumwosha mtoto.
  • Baada ya kumbadilisha mtoto nepi na kutupa kinyesi.
  • Baada ya mama kubadilisha padi zake mwenyewe zinazotumika kufyonzea mchozo wa damu kutoka ukeni.
  • Baada ya kutumia choo.
  • Kabla au baada ya kuandaa chakula.

Unapoendelea kunawa mikono, mwambie mama aanze kunyonyesha. (Katika Kipindi kijacho, tutakufunza kwa kina kuhusu utaratibu mwafaka wa kunyonyesha). Mama anaponyonyesha, utachukua fursa hiyo kubaini kama kuna matatizo yoyote yanayohusiana na kunyonyesha. Kunyonyesha pia humtuliza mtoto unapomchunguza. Iwapo mtoto atalia unapomchunguza, Malengo ya uchunguzi huo yanaweza kuathirika. Hivyo basi, jaribu kila mara kuwatuliza watoto unapowachunguza.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 6

6.2 Kumkagua mtoto ili kubaini dalili hatari za kijumla