6.2 Kumkagua mtoto ili kubaini dalili hatari za kijumla

Katika ziara ya kwanza, jambo muhimu zaidi ni kuwachunguza watoto wote Wachanga ili kubaini uwepo wa dalili hatari za kijumla katika watoto Wachanga (Kisanduku 6.1). Dalili hizi tayari zimeorodheshwa kwa kifupi katika Kipindi cha 1. Kila wakati, kumbuka kuzingatia uangalifu, wepesi wa kutambua na utaratibu unapomchunguza na kumhudumia mtoto mchanga, hasa katika siku za kwanza za uhai wake. Pia, muda wote unapomhudumia mama na mtoto mchanga, unashauriwa kuwa makini ili kutambua uwezekano wa kuwepo kwa dalili kuu hatari.

Matatizo yanayohusiana na kula yamezungumziwa kwa kina katika Kipindi cha 7.

Kisanduku 6.1 Dalili hatari za kijumla kwa watoto Wachanga

  • Historia ya ugumu wa kula, au mtoto hawezi kula kwa sasa - muulize mama kuhusu jinsi mtoto anavyokula.
  • Historia ya mitukutiko, au mtoto anatukutika kwa sasa - muulize mama kama mtoto ameshawahi kupata mitukutiko ya maungo.
  • Mtoto mchanga anaonekana mlegevu au amepoteza fahamu.
  • Mtoto anasonga tu iwapo amesisimuliwa.
  • Kupumua kwa haraka.
  • Kifua kubonyea ndani sana.
  • Homa.
  • Hipothemia (ukimguza, unahisi kuwa mtoto ana baridi)
  • Mtoto amekuwa na rangi ya manjano kabla ya kufikisha umri wa saa 24. Umanjano unaoonekana kwenye viganja vya mikono na nyayo za miguu.
  • Macho yamefura au yanatoa mchozo.
  • Usaha unatoka kitovuni.
  • Zaidi ya pustuli (madoa) 10 zinaonekana ngozini.

6.1 Hatua za kwanza kabla ya kumchunguza mtoto mchanga

6.2.1 Je, unaweza kutambua vipi kuwa mtoto mchanga ana mtukutiko?