6.2.1 Je, unaweza kutambua vipi kuwa mtoto mchanga ana mtukutiko?

Apnea ni dalili hatari sana. Iwapo unakisia kuwa mtoto amepata mtukutiko, au unatambua dalili za mtukutiko wakati wa ziara, mpe mama na mtoto rufaa ya dharura hadi katika kituo cha hali ya juu cha afya.

Katika mtoto mchanga, mtukutiko (mtukutiko wa maungo) unaweza kudhihirika kama:

  • Mtetemo wa kiungo cha mwili (kama vile mkono), sehemu ya mwili, au mwili wote (mtukutiko wa mwili wote).
  • Mtandaziko wa (spazimu ya) kiungo cha mwili (kama vile mkono) au mwili wote.
  • Miendo isiyo ya kawaida (kama vile ya mdomo, kugeuza macho upande mmoja au miendo ya miguu kana kwamba anaendesha baiskeli).
  • Apnea (vipindi virefu vya kukosa kupumua).

Mara nyingi ni vigumu kutambua mtukutiko katika watoto Wachanga kwa sababu mwili na viungo vyao havitandaziki kwa pamoja au mwili kushtuka kama ilivvyo kwa mitukutiko ya watoto wakubwa na watu wazima. Kwa hivyo, ni muhimu sana kuwa makini ili kutambua dalili zozote zisizo za kawaida, hata kama dalili hizi si wazi mwanzoni.

6.2 Kumkagua mtoto ili kubaini dalili hatari za kijumla

6.2.2 Je, mtoto mchanga amelegea au amepoteza fahamu?