6.2.2 Je, mtoto mchanga amelegea au amepoteza fahamu?

Mtoto aliyepoteza ufahamu anafaa kupelekwa rufaa kwenye kituo cha afya mara moja.

Tazama miendo ya mtoto huyu mchanga. Je, mtoto anacheza kama inavyotarajiwa kwa mtoto mwenye afya bora au la? Je, mtoto anachezesha viungo anapochangamshwa tu (amelegea?) Iwapo mama amewahi kuzaa tena, au kina mama wengine wenye tajiriba wako mle nyumbani, waulize kama wanafikiri mtoto huyu amelegea. Iwapo mtoto hachezeshi viungo au hajibizi changamsho kama kawaida, basi yuko katika hatari.

6.2.1 Je, unaweza kutambua vipi kuwa mtoto mchanga ana mtukutiko?

6.2.3 Je, mtoto huyu anapumua kwa kasi sana?