6.2.3 Je, mtoto huyu anapumua kwa kasi sana?

Mpe rufaa mtoto anayeonekana kuwa na matatizo ya kupumua.

Hesabu idadi ya kadri mtoto anavyopumua kwa dakika moja. Je, anapumua kama kawaida au kwa kasi sana? Kupumua kwa kasi ni kupumua mara 60 au zaidi kwa dakika. Mtoto mchanga hupumua mara 40 - 60 kwa dakika. Kimo hiki hupimwa mara mbili kwa kipindi cha dakika moja kila wakati. Chunguza ili utambue kama mtoto ana kifua kinachobonyea sana. Hii inamaanisha kuwa mtoto anapovuta pumzi, sehemu ya chini mwa mbavu ‘hufyonzeka’ ndani sana (Mchoro 6.2).

Mchoro 6.2 Kubonyea kwa kifua ni dalili kuwa mtoto mchanga ana matatizo ya kupumua.

6.2.2 Je, mtoto mchanga amelegea au amepoteza fahamu?

6.2.4 Je, jotomwili la mtoto ni la kawaida?