6.2.4 Je, jotomwili la mtoto ni la kawaida?

Pima kiwango cha jotomwili la mtoto, hasa ukitumia themometa iliyoingizwa taratibu kwenye rektamu kupitia kinyeoni, au utumie themometa ya kawaida iliyoshikiliwa taratibu kwapani mwa mtoto (hii hujulikana kama jotomwili la kwapani). Kumbuka kuwa themometa hii inafaa kuwa safi kabisa kabla ya kuitumia. Ioshe themometa kwa maji safi kabla na baada ya kuitumia, kisha uisugue kwa swabu iliyolowa alkoholi au kiowevu kingine cha kutakasa. Iwapo hauna themometa, tumia mkono wako kuguza kichwa na mwili wa mtoto kubaini kama ana homa au kiwango cha chini cha jotomwili. Hii ni kwa kulinganisha hali ya mtoto na yako au ngozi ya mama.

Mpe rufaa mtoto aliye na homa au hipothemia, iwapo kiwango chake cha jotomwili hakijarejea hali ya kawaida upesi.

Homa hufasiliwa kama kiwango cha jotomwili cha nyusi 37.5 au zaidi. Iwapo unakisia kuwa mtoto ana joto jingi kutokana na joto la mama, mpunguzie joto kwa kuondoa blanketi zake kisha upime kiwangojoto tena baada ya dakika 15. Iwapo kiwango cha jotomwili hakitarejea hadi kawaida kwa upesi, au kinazidi nyusi 37.5, mpeleke rufaa haraka. Kiwango cha juu cha jotomwili ni dalili hatari ya maambukizi, ambayo yanafaa kutibiwa haraka. Habari zaidi kuhusu maambukizi ya mtoto mchanga zimepeanwa katika Kifungu 6.4 cha Kipindi hiki.

Mchoro 6.3 Njia bora zaidi ya kumpasha joto mtoto aliye na baridi ni kumshika huku mwili wake ukiguzana moja kwa moja na wa mama.

Hipothemia hufasiliwa kama kiwango cha jotomwili cha nyusi 35.5 au zaidi, ingawa kiwango hiki ni cha chini sana na hatari kwa mtoto mchanga. Iwapo mtoto ana baridi, usigonje kiwangojoto kishuke hadi chini ya nyusi 36.5 kabla ya kuchukua hatua ya dharura ili kumpasha joto. Mvue nguo kisha umweke huku mwili wake ukiguzana na wa mama, katikati ya matiti akiwa amefunikwa kwa nguo. (Mchoro 6.3) Mfunike mama na mtoto kwa blanketi, huku ukifunika kichwa cha mtoto kwa chepeo au kijiblanketi. Iwapo mtoto hajavishwa sokisi, ifunike miguu yake (hii hujulikana kama Utunzaji wa Mama wa aina ya Kangaruu, kama utakavyojifunza katika Kipindi cha 8.) Iwapo kiwango cha jotomwili cha mtoto hakianzi kupanda hadi kile cha kawaida baada ya dakika 30, au ki chini ya nyusi 35.5, au midomo ya mtoto ni ya rangi ya samawati, mpeleke mtoto rufaa mara moja.

Baada ya kumchunguza mtoto ili kutambua dalili kuu kama ilivyoelezwa hapo juu, hatua inayofuata ni kumchunguza ili kutambua dalili hatari za maradhi ya watoto Wachanga.

6.2.3 Je, mtoto huyu anapumua kwa kasi sana?

6.3 Je, mtoto ana umanjano?