6.3 Je, mtoto ana umanjano?

Dalili za maradhi ya umanjano ni uwepo wa rangi ya manjano ngozini na kwenye sklera (sehemu nyeupe ya macho). Hata hivyo, ni vigumu kuiona sklera ya watoto Wachanga, basi rangi ya ngozi hutumika kutambua umanjano. Kwanza muulize mama kama aliona rangi yoyote ya manjano ngozini mwa mtoto kabla hajafikisha umri wa saa 24. Baada ya hilo, chunguza mwenyewe huku ukikadiria kama viganja vya mikono na nyayo za miguu zina rangi ya manjano. Umanjano husababishwa na wingi wa hakiba ya pigmenti za manjano zinazojulikana kama bilirubini (hali hii pia hujulikana kama hipabilirubinemia, ‘bilirubini iliyopita kiasi’). Umanjano hujitokeza ngozini wakati hemoglobini kupita kiasi (protini inayobeba oksijeni) na iliyo katika seli nyekundu za damu imemenywa, au wakati ini halitendi kazi vyema, hivyo haliwezi kupunguza bilirubini, au wakati mshipa wa kutoa nyongo umezibwa. (Nyongo ni kiowevu kinachosaidia kumenya bilirubini na ambacho hutoleshwa na tezi za nyongo).

Mtoto mchanga asipotibiwa, bilirubini iliyopita kiasi huathiri sana ubongo wake, na hata kusababisha kifo. Isipotibiwa, inaweza kusababisha matatizo ya muda mrefu ya neva (matatizo yanayohusiana na kuathiriwa kwa mfumo wa kati wa neva, kama vile kupooza kwa baadhi ya sehemu za mwili, msoto au ugumu wa kujifunza)

6.2.4 Je, jotomwili la mtoto ni la kawaida?

6.4 Maambukizi kwa mtoto mchanga