6.4 Maambukizi kwa mtoto mchanga

Maambukizi hutokea mara nyingi katika watoto Wachanga. Maambukizi haya ni baadhi ya visababishi vikuu vya vifo vya watoto.

  • Je, unaweza kukumbuka (kwa mfano, kwa kurejelea Kipindi cha 1) ni kwa nini kuna hatari zaidi ya watoto Wachanga kuambukizwa ikilinganishwa na watoto wakubwa au watu wazima?

  • Sababu moja kuu ni kutokomaa kwa mfumo wa kinga ya mwili. Utaratibu huu huchukua miezi kadhaa baada ya kuzaliwa hadi kufikia kiwango cha kuukinga mwili dhidi ya maambukizo.

    Mwisho wa jibu

Kipindi cha 17, Moduli ya Utunzaji katika ujauzito kinafunza kuhusu kupasuka kwa membreni za fetasi kabla ya wakati. Habari kuhusu leba inayochukua muda mrefu au iliyokinzana imetolewa katika Kipindi cha 9 cha Moduli ya Utunzaji wa Leba na Kuzaa.

Hii inamaanisha kuwa watoto Wachanga wako katika hatari kuu zaidi ya kuathiriwa na viini vya maambukizi wakati wa ujauzito, wanapozaliwa nyumbani na baada ya kuzaliwa. Vipengele vinavyosababisha hatari zaidi kwa watoto Wachanga ni wakati membreni za fetasi zimepasuka muda mrefu kabla ya wakati, leba imechukua muda mrefu, na maambukizi ambayo yamekuwepo katika sehemu ya chini ya njia ya uke wa mama. Kwanza tuzingatie maambukizi ya macho kwa watoto Wachanga.

6.3 Je, mtoto ana umanjano?

6.4.1 Je, dalili za maambukizi ya macho ni gani?