6.4.1 Je, dalili za maambukizi ya macho ni gani?

Iwapo njia ya uzazi ya mama ina bakteria zinazosababisha magonjwa ya zinaa (hasa klamidia na kisonono), viini vya maambukizi haya vinaweza kuingia machoni mwa mtoto wakati wa kuzaliwa na hivyo vinaweza kusababisha upofu. Chunguza ubaini kama kuna uvimbe wa kope, wekundi kwenye sehemu ya ndani ya macho au mchozo kutoka machoni. Unaweza kumpa profilaksisi (matibabu ya kuzuia maambukizi) punde anapozaliwa. Matibabu haya yanaweza kufanywa kwa kutumia tetracycline au lihamu nyingine ya macho iliyopendekezwa, kama ilivyoonyeshwa katika Mchoro 6.4. Lakini iwapo mtoto huyu ameambukizwa macho baada ya kuzaliwa, mpeleke rufaa hadi hospitalini au katika kituo cha afya kwa uchunguzi au matibabu ya kina.

Mchoro 6.4 Desturi iliyopo ya kutunza macho ya mtoto mchanga ili asiambukizwe ni kupaka tetracycline mara moja punde baada ya kuzaliwa.

6.4 Maambukizi kwa mtoto mchanga

6.4.2 Je, dalili za maambukizi ya kiungamwana ni gani?