6.4.2 Je, dalili za maambukizi ya kiungamwana ni gani?

Mpeleke rufaa hadi hospitalini au kituoni mtoto anayeonyesha dalili zozote za maambukizi ya kitovu. Usitumie poda ya antibayotiki. Usimtie asprin kitovuni, wala dawa zozote za kutayarishiwa nyumbani.

Chunguza kiungamwana: je, ni chekundu au kinatoa usaha? Maambukizi ya kitovu huonyesha dalili hatari zifuatazo:

  • Kiungamwana kinachotoa uvundo na usaha.
  • Kiungamwana kinachobakia laini na chenye unyevunyevu na wala hakikauki vyema.
  • Wekundu wa ngozi inayozunguka mzizi wa kitovu.

Utunzaji bora wa kiungamwana unaweza kuzuia kutokea kwa maambukizi ya kiungamwana. Kinga dhidi ya maambukizi hujumuisha:

  • Kunawa mikono vyema
  • Usafi bora wa kibinafsi, wa mama na mtoto
  • Kufunga kiungamwana kwa uzi safi uliotakaswa na kukikata kwa vifaa vilivyotakaswa
  • Kuhakikisha kuwa kitovu ni safi na kikavu

6.4.1 Je, dalili za maambukizi ya macho ni gani?

6.4.3 Je, dalili za maambukizi ya ngozi ni gani?