6.4.3 Je, dalili za maambukizi ya ngozi ni gani?

Aina mbili kuu za maambukizi ya ngozi ya mtoto mchanga ni:

Mpeleke rufaa hadi hospitalini au kituoni mtoto anayeonyesha dalili za impetigo au upele wa moniliaisisi.

  • Maradhi ya impetigo husababishwa na bakteria iitwayo Staphylococcus iliyo ngozini. Maradhi haya hujitokeza kama uvimbe wenye usaha (pustuli) na kwa kawaida huonekana yamekizunguka kitovu au sehemu inayofungwa nepi. Je, kuna pustuli zozote? Pustuli zaidi ya 10 ni dalili ya kijumla ya hatari.
  • Upele wa moniliasisi husababishwa na fangasi (za daraja la Kandida au Monila). Mara nyingi, maradhi haya hutokea katika sehemu inayofungwa nepi. Dalili zake ni madoadoa mekundu yaliyofura kidogo, na yaliyokithiri mikunjoni mwa ngozi.

Kinyume na haya, upele unaotokana na nepi unaosababishwa na muwasho wa ngozi kwa sababu ya mkojo au kinyesi kwa kawaida huathiri sehemu wazi za ngozi wala sio mikunjo. Iwapo upele huu haujaambatana na maambukizi, kwa kawaida utadhibitiwa kwa kudumisha usafi wa hali ya juu, kumwosha mtoto mara nyingi kwa maji vuguvugu na kuacha ngozi ikauke kabisa.

Upele unaotokana na jasho, unaosababishwa na kutoa jasho jingi, unaweza kufanana na maambukizi, lakini sio maambukizi. Upele huu hujitokeza kwenye paji la uso kama vimbe dogo zisizo na rangi yoyote, au upele mwekundu kabisa shingoni na katika kiwiliwili. Mhakikishie mama kuwa hili si tatizo kuu, kisha umshauri amwoshe mtoto kwa maji vuguvugu na amkinge kutokana na joto jingi.

6.4.2 Je, dalili za maambukizi ya kiungamwana ni gani?

6.4.4 Tetanasi ya watoto Wachanga ni nini?