6.4.4 Tetanasi ya watoto Wachanga ni nini?

Mhamishe kwa darura mtoto aliye na dalili za tetanasi hadi hospitalini au kituo cha afya kilicho karibu. Mkiwa safarini, mkinge mtoto kutokana na hipothemia na umpe maziwa ya mama.

Tetanasi inayoathiri watoto Wachanga husababishwa na bakteria (Clostridium tetani) inayoambukiza tishu zilizokufa kama vile kitovu. Bakteria za tetanasi hupatikana kwenye udongo na kinyesi cha wanyama. Bakteria hizi zinaweza kuambukiza kiungamwana au vidonda vingine, kama vile kupitia desturi hatari za kimila. Bakteria hizi hutoa toksini (sumu) kali zinazoathiri mfumo wa neva. Itakisiwa kuwa mtoto ana tetanasi iwapo ataonyesha dalili zifuatazo:

  • Kuongezeka kwa mikazo ya misuli (spazimu), hususan katika misuli ya taya na fumbatio.
  • Spazimu ya misuli ya mwili wote na mtukutiko wa maungo unaosababishwa na vichocheo kama vile kushikwa au kelele. Mtoto anaweza kujipinda nyuma wakati wa spazimu (Kielelezo 6.5)
  • Watoto wengi walioambukizwa tetanasi hukumbwa na ugumu wa kupumua na wengi hufa hata wakiwa wamehudumiwa kimatibabu.
Mchoro 6.5 Mfano dhahiri wa spazimu ya misuli ya mtoto mchanga aliyeambukizwa tetanasi

6.4.3 Je, dalili za maambukizi ya ngozi ni gani?

6.4.5 Utawakinga vipi watoto wachanga dhidi ya maambukizi ya tetanasi?