6.5 Orodha ya kukadiria hali hatari ya watoto wachanga

Baada ya kumuuliza mama kuhusu matatizo yoyote ya mtoto mchanga na kufanya uchunguzi wa kimsingi wewe mwenyewe, unaweza kumuainisha mtoto kulingana na orodha ya uchunguzi inayofuata (Jedwali 6.1).

Baada ya kumchunguza mtoto ili kubaini hali tata, kumbuka kuchunguza tena kuhusu dalili zote sizizo za kawaida alizozaliwa nazo/au dalili zote za majeraha ya wakati wa kuzaliwa (kwa mfano hitilafu mgongoni, kufura kwa kichwa, vilia vingi). Dalili hizi zinaweza kusababisha uhaba wa ghafla wa damu hivyo kupelekea kutokea kwa anemia.

Katika Kipindi cha 7, tutaeleza yote ambayo inakupasa wewe na mama kufahamu kuhusu kunyonyesha. Kubaini kuwa mtoto ananyonya vizuri na mama anaweza kumnyonyesha inavyofaa ni lengo moja la ziara ya nyumbani ya baada ya mama kuzaa. Unapaswa pia kumpima mtoto uzani kila mara unapomzuru nyumbani ili kuhakikisha kuwa anaongeza uzani kikawaida. Jambo hili ni muhimu hasa kwa watoto waliozaliwa kabla ya wakati (wiki 37 hadi 42 za ujauzito), au wale waliozaliwa na uzani wa chini ya kiwango cha kawaida (sawa na au zaidi ya gramu 2,500).

Watoto waliozaliwa kabla ya kukamilika kwa kipindi cha ujauzito (waliozaliwa katika wiki ya 32 – 36 ya ujauzito), watoto waliozaliwa muda mrefu kabla ya kukamilika kwa kipindi cha ujauzito (walizaliwa kabla ya wiki 32 za ujauzito), na watoto walio na uzani wa chini (chini ya gramu 1,500) wanaweza kuwa na dalili hatari za ziada kwa sababu hawajapata uwiano wa kumeza na kupumua, hivyo hawawezi kunyonya vyema. Utajifunza kuhusu utunzaji maalum wa watoto hawa wadogo sana katika Kipindi cha 8.

Jedwali 6.1 Orodha ya uchunguzi wa watoto Wachanga: chati ya ‘kuchunguza na kuainisha.
Uliza na uchunguzeAinishaHatua
  • Historia ya ugumu wa kunyonya au hawezi kunyonya sasa.
  • Historia ya mtukutiko wa maungo au anatukutika maungo sasa.
  • Mtoto mchanga ni mlegevu au amepoteza fahamu.
  • Mwendo hutendeka tu anapochochewa.
  • Kupumua kwa kasi
  • Kubonyea sana kwa sehemu ya chini ya kifua
  • Homa
  • Hipothemia

Ikiwa kuna mojawapo ya dalili hizi hatari za kijumla, ainisha kama:

MAAMBUKIZI HATARI YANAYOWEZA KUWEPO

Hamisha mtoto KWA DARURA hadi hospitalini au kituo cha afya

Hakikisha mtoto amepashwa joto la kutosha na umpe maziwa ya mama mkiwa safarini.

  • Mtoto kubadilika na kuwa manjano kabla ya saa 24 za umri wake.
  • Umanjano katika viganja na nyayo.
  • Kufura kwa macho au mchozo kutoka machoni.
  • Kutokwa na usaha kitovuni
  • Kupatikana kwa pustule zaidi ya 10 kwenye ngozi
  • Hakuna dalili zozote zilizotajwa hapo juu.

Ikiwa kuna mojawapo ya dalili hizi hatari, ainisha kama:

MAAMBUKIZI YANAYOWEZA KUWEPO AU UMANJANO

Hamisha mtoto KWA DARURA hadi hospitalini au kituo cha afya

Hakikisha mtoto amepashwa joto la kutosha na umpe maziwa ya mama mkiwa safarini.

MTOTOASIYE NA MATATIZOKumnyonyesha na kumtunza ili kumkinga dhidi ya maambukizi na kuhakikisha amepata joto la kutosha.

6.4.5 Utawakinga vipi watoto wachanga dhidi ya maambukizi ya tetanasi?

Muhtasari wa Kipindi cha 6