Muhtasari wa Kipindi cha 6

Katika Kipindi cha 6 umejifunza kuwa :

  1. Lengo muhimu la ziara yoyote ya nyumbani ni kumchunguza mtoto mchanga ili kubaini dalili zote za hatari, zikiwemo: kukosa kunyonya, mtukutiko wa maungo, ulegevu au mwendo wa mwili usio wa kawaida, kupumua kwa kasi na kubonyea kwa kifua, vidonda vya ngozi vikiwemo maambukizi ya kitovu, mchozo machoni na tetanasi ya mtoto mchanga.
  2. Maandalizi yanayofanywa kila mara kabla ya kumchunguza mtoto ni kunawa mikono yako vyema na kumuagiza mama aanze kunyonyesha ili uchunguze jinsi mtoto anavyonyonya, na pia kumtuliza mtoto unapoendelea kumchunguzi.
  3. Kumuuliza mama hali ya mtoto wake ni jambo muhimu linalokupasha habari utakayotumia katika uchunguzi.
  4. Hakikisha umemwelezea mama njia anazoweza kutumia kuzuia mtoto wake kuambukizwa, ikiwa ni pamoja na kunawa mikono, kuhakikisha mtoto ni safi, na kwamba kitovu ni safi na kimekauka. Pia anafaa aepukane na msongamano au hali zisizo safi katika mahali wanamoishi.
  5. Kulingana na chati ya ‘Chunguza na Uainishe’ (Jedwali 6.1), orodha zinazoweza kupatikana ni: uwezekano wa maambukizi hatari, uwezekano wa maambukizi au umanjano, au mtoto asiyeambukizwa. Uainishaji utakusaidia kufanya uamuzi wa busara kuhusu hatua utakayochukua.

6.5 Orodha ya kukadiria hali hatari ya watoto wachanga

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 6