Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 6

Kwa kuwa sasa umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili linatathmini jinsi ulivyojifunza. Kwanza, soma Mfano 6.1 kisha uyajibu maswali yanayofuata.

Mfano 6.1 Uchunguzi wa mtoto mchanga wa kike

Mtoto wa kike alizaliwa na mama wa umri wa miaka 32 katika kipindi cha wiki 39 za ujauzito. Ulimchunguza mtoto saa 28 baada ya kuzaliwa. Ana uzani wa kuzaliwa wa gramu 3,000 na ana historia ya mtukutiko wa maungo. Mtoto huyu pia hawezi kabisa kunyonya na kiwango chake cha jotomwili ni nyusi 38.5

Maswali la Kujitathmini 6.1(yanatathmini Malengo ya Somo la 6.1 na 6.3)

  • a.Utamuainishaje mtoto huyu ukizingatia umri wake wa ujauzito?
  • b.Utamuainishaje kulingana na uzani wake wa kuzaliwa?
  • c.Orodhesha dalili jumla za hatari zinazodhiirishwa na mtoto huyu.
  • d.Je una wazo gani kuhusu kiwago cha joto cha mwili cha mtoto huyu?
  • e.Utatoa uainisho gani wa tamati kuhusu mtoto huyu na jinsi gani utadhibiti hali yake?

Answer

  • a.Katika wiki 39 za ujauzito, mtoto huyu huainishwa kama mtoto aliyehitimu muhula wa kawaida.
  • b.Uzani wa kuzaliwa ni gramu 3,000, ambao huainishwa kama uzito wa kawaida wa kuzaliwa
  • c.Dalili hatari za jumla ni: kutonyonya, historia ya mtukutiko wa maungo na joto jingi mwilini.
  • d.Kiwango cha jotomwili (nyusi 38.5) si cha kawida na mtoto ana homa. Kiwango cha jotomwili cha kawaida kwa mtoto mchanga ni zaidi ya nyusi 36.5 hadi chini ya nyusi 37.5
  • e.Mtoto huyu ana dalili tatu kuu za hatari (kutonyonya, mtukutiko wa maungo na homa) na huainishwa kama aliye na uwezekano wa maambukizi. Njia iliyo bora ya kumhudumia mtoto huyu ni kumhamisha kwa dharura hadi hospitalini au katika kituo cha afya huku ukipendekeza kuwa mtoto amepata joto la kutosha na kumpa maziwa ya mama mkiwa safarini.

Mwisho wa jibu.

Sasa soma Mfano 6.2 kisha uyajibu maswali yanayofuata

Mfano 6.2 Uchunguzi wa mtoto mchanga wa kiume

Unamchunguza mtoto mchanga wa kiume mwenye umri wa saa nane, aliyezaliwa na mama mwenye umri wa miaka 27 katika kipindi cha wiki 31 za ujauzito. Mama huyu alikuwa anazaa kwa mara ya kwanza. Mtoto huyu ana uzani wa kuzaliwa wa gramu 1,300, anadhiirisha kima cha pumzi cha mara 72 kwa dakika na kifua kinabonyea. Kiwango cha jotomwilini nyusi 34.5

Maswali ya Kujitathmini 6.2 (yanatathmini Malengo ya Somo la 6.1 na 6.3)

  • a.Utaainisha vipi umri wa ujauzito wa mtoto huyu?
  • b.Utaainisha vipi mtoto huyu kulingana na uzani wake wa kuzaliwa?
  • c.Je kima cha pumzi mara 72 kwa dakika ni cha kawaida au la? Je kupumua kawaida ni kwa kiwango gani?
  • d.Je kuna nini kuhusu kiwango cha jotomwili cha mtoto huyu ni cha kawaida?
  • e.Utamdhibiti vipi mtoto huyu?

Answer

  • a.Kwa sababu mtoto alizaliwa akiwa na wiki 31 ya ujauzito, ataainishwa kama aliyezaliwa muda mrefu kabla ya wakati.
  • b.Uzani wa kuzaliwa ni gramu 1300, hivyo ataainishwa kama aliye na uzani wa kuzaliwa wa chini mno.
  • c.Kima chake cha pumzi cha mara 72 kwa dakika si cha kawaida. Mtoto huyu anapumua kwa kasi. Kima cha kawaida cha kupumua ni mara 40-60 kwa dakika.
  • d.Kiwango cha jotomwili (nyusi 34.5) ki chini mno. Mtoto ana hipothemia. Kiwango joto cha kawaida cha mtoto mchanga ni juu ya nyusi 36.5 hadi chini ya nyusi 37.5.
  • e.Kwa sababu alizaliwa muda mrefu kabla ya wakati na yuko na uzani wa chini sana, pia akiwa na dalili mbili kuu za hatari (kupumua kwa kasi na hipothemia), mtoto huyu anaainishwa kama aliye na uwezekano wa kuambukizwa. Hatua abora ya kumhudumia ni kumhamisha kidharura hadi hospitalini au katika kituo cha afya ukipendekeza hakikisho la kuwa mtoto amepata jotola kutosha na kumpa maziwa ya mama wakiwa safarini.

Mwisho wa jibu.

Maswali ya Kujitathmini 6.3 (yanatathmini Malengo ya Somo la 6.1, 6.2 na 6.4)

Tuseme ni siku yako ya kwanza kumzuru mama aliyezaa salama. Unamchunguza mtoto mchanga kama yuko salama, ikiwemo kuchunguza dalili za maambukizi.

  • Utamuuliza nini mama kabla ya kuanza kumchunguza mtoto mchanga?
  • Ni kitu gani utakachohakikisha kubaini utakapokuwa ukimchunguza mtoto huyu?

Tumia Jedwali 6.2 lililo hapa chini ili kupanga majibu yako

Jedwali 6.2 Kumchunguza mtoto mchanga
Maswali kwa mamaVitu vya kuchunguza katika mtoto mchanga

Answer

Jedwali 6.2 Kumchunguza mtoto mchanga (Jedwali lililokamilishwa).
Maswali utakayomuuliza mamaVitu vya kuchunguza katika mtoto mchanga
Je, mama anakumbuka kunawa mikono kabla ya kunyonyesha na kuzingatia usafi wake na wa mtoto?Je mama na mtoto wanaonekana safi na wazima. Je chumba ki safi na nadhifu?
Je mama amegundua mwendo wowote usio wa kawaida, spazimu ya mkono au mwili wote?Ikiwa ndivyo, chunguza kwa makini kubaini ikiwa mtoto anaweza kuwa ana mtukutiko wa maungo
Je mtoto anapumua taratibu bila ugumu?Kama mama ana wasiwasi, chunguza kuhusu kubonyea kwa kifua (kifua cha mtoto kubonyea ndani katika mbavu za chini) pia chunguza dalili za mtukutiko wa maungo.
Je mama anatunza kitovu kwa kuhakikisha ni safi na kimekauka? Je amegundua uvundo wowote kutoka kitovuni?Chunguza kama kuna mchozo au wekundu wa ngozi uliozunguka kitovu. Mkumbushe mama umuhimu wa kutunza kitovu kwa kuhakikisha ni safi na kimekaushwa.
Je, amegundua wekundu wowote au uozo kutoka kwa macho ya mtoto?Je tetracycline (au dawa yoyote ile ya macho iliyoidhinishwa) ilipakwa machoni mwa mtoto alipozaliwa.
Je mtoto anonekana mwenye baridi au mwenye joto jingi?Ikiwa mtoto anaonekana mwenye joto jingi, pima kiwango chake cha jotomwili (kwa kutumia themometa safi) na pia uchunguze kama amefunikwa vizuri. Ikiwa yuko baridi, chunguza kama ana hipothemia.
Je mama ana tatizo lolote akinyonyesha? Ikiwa ndivyo, chunguza kama chuchu za mama zimepasuka au ana joto jingi katika matiti (mastitisi au jipu). Kama anasita kunyonyesha mkumbushe umuhimu wa maziwa kwa mtoto, kwani yana virutubishi na hukinga mtoto dhidi ya maambukizi.
Je mtoto ana dalili zozote za upele? Ikiwa ndivyo, ni upele unaohusiana na nepi au jasho? Je kuna pustuli (malengelenge yenye usaha) ikiwa ni hivyo, malengelenge hayo yanazidi 10?
Je, yeye au mtoto alifanyishwa tambiko lolote hatari la kitamaduni kufuatia uzazi?Ikiwa ndivyo, chunguza mtoto kubaini dalili zozote za tetanasi (k.m spazimu ya misuli) na umwulize mama kama amechanjwa dhidi ya tetanasi.
Je mama anajihisi mzima kwa kijumla? Je, anakabiliana vyema na changamoto za kumtunza mtoto mchanga?Je mama anapata usaidizi wa kutosha, na mtoto anapata utunzaji wote anaohitaji?

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 6