Malengo ya Somo la Kipindi cha 7

Baada ya Kipindi hiki, unafaa kuweza;

7.1 Kufafanua na kutumia kwa ufasaha maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (Swali la Kujithamini 7.2)

7.2 Kueleza faida za maziwa ya mama kwa mtoto mchanga na umuhimu wa unyonyeshaji wa kipekee kwa mama na mtoto mchanga. (Swali la Kujitathmini 7.1)

7.3 Kuelezea hatua za kuanzisha unyonyeshaji bora kupitia njia nzuri ya mama kuketi na namna ya kumweka mtoto kwa matiti yake. (Swali la Kujitathmini 7.2)

7.4 Kuelezea jinsi ya kumshauri mama aliye na VVU kuhusu aina za ulishaji ili mtoto wake apunguze hatari ya kuambukizwa VVU kupitia maziwa ya mama. (Swali la Kujitathmini 7.1)

7.5 Kuelezea jinsi watoto wachanga hupoteza joto na jinsi ya kuzuia hipothemia kwa kutumia kanuni ya mfululizo joto

Kipindi cha 7 Unyonyeshaji, kanuni ya mfululizo joto na kuwapa ushauri kina Mama walio na virusi vya ukimwi (VVU)

7.1 Kumpa ushauri mama kuhusu ulishaji wa mtoto mchanga