7.1.1 Ishara nne nzuri za mama kukaa
Jambo la kwanza ni mama kuketi kwa utulivu (tazama Mchoro 7.1a) na kudumisha ishara nne nzuri za kuketi
- Kichwa na mwili wa mtoto mchanga uwe laini
- Mtoto mchanga atazame matiti yake na pua lake liwe kinyume cha chuchu
- Mwili wa mtoto mchanga iwe karibu na ya mama
- Mama anashikilia mwili wote wa mtoto bali sio shingo na mabega pekee yake.
Ikiwa mama amewahi kufanyiwa upasuaji wakati wa kuzaa au fumbatio lake ni uchungu kwa sababu nyinginezo, anaweza kuwa na starehe akimshikilia mtoto kama inavyoonyeshwa katika Mchoro 7.1(b). Inaweka uzito wa mtoto mbali na fumbatio lake. Anaweza kulisha mapacha hivi pia, kila mmoja na titi lake. Usiku au ikiwa amechoka na anahitaji kupumzika, anaweza kumlisha mtoto akiwa amelala chini (Mchoro 7.1c), lakini ikiwa atabaki macho tu.
Kunyonyeshaji ukiwa umelala chini (Mchoro 7.1c) sio nzuri isipokuwa tu mama akiwa macho tu. Unaweza kupendekeza ni kwa nini?
Ikiwa mama atalala, anaweza kumlalia mtoto mchanga ambaye anaweza kuwa hana uwezo wa kupumua na ukosefu wa hewa (kufa kutokana na oksijeni)
Mwisho wa jibu
7.1 Kumpa ushauri mama kuhusu ulishaji wa mtoto mchanga