7.1.1 Ishara nne nzuri za mama kukaa

Jambo la kwanza ni mama kuketi kwa utulivu (tazama Mchoro 7.1a) na kudumisha ishara nne nzuri za kuketi

  • Kichwa na mwili wa mtoto mchanga uwe laini
  • Mtoto mchanga atazame matiti yake na pua lake liwe kinyume cha chuchu
  • Mwili wa mtoto mchanga iwe karibu na ya mama
  • Mama anashikilia mwili wote wa mtoto bali sio shingo na mabega pekee yake.

Ikiwa mama amewahi kufanyiwa upasuaji wakati wa kuzaa au fumbatio lake ni uchungu kwa sababu nyinginezo, anaweza kuwa na starehe akimshikilia mtoto kama inavyoonyeshwa katika Mchoro 7.1(b). Inaweka uzito wa mtoto mbali na fumbatio lake. Anaweza kulisha mapacha hivi pia, kila mmoja na titi lake. Usiku au ikiwa amechoka na anahitaji kupumzika, anaweza kumlisha mtoto akiwa amelala chini (Mchoro 7.1c), lakini ikiwa atabaki macho tu.

Mchoro 7.1 (a) Mama huyu yuko katika hali nzuri ya unyonyeshaji bora (b)Hii ni hali nzuri ya kunyonyesha wakati mama amefanyiwa upasuaji wa fumbatio, au ikiwa analisha mapacha. (c) Mtoto anaweza kulishwa akilala chini, lakini ikiwa mama yuko macho.
  • Kunyonyeshaji ukiwa umelala chini (Mchoro 7.1c) sio nzuri isipokuwa tu mama akiwa macho tu. Unaweza kupendekeza ni kwa nini?

  • Ikiwa mama atalala, anaweza kumlalia mtoto mchanga ambaye anaweza kuwa hana uwezo wa kupumua na ukosefu wa hewa (kufa kutokana na oksijeni)

    Mwisho wa jibu

7.1 Kumpa ushauri mama kuhusu ulishaji wa mtoto mchanga

7.1.2 Ishara nne nzuri za uhusiano mzuri