7.2.1 Manufaa ya unyonyeshaji kwa mtoto mchanga

Maziwa ya titi ni lishe kuu lililo bora kwa watoto kwa kuwa humpa virutubishi vyote kwa kiasi na ulinganisho sahihi kwa maendeleo na ukuaji wa kawaida hadi kufikia miezi sita. Hufyonzwa na kumeng’eywa kwa urahisi. Pia maziwa ya titi ni safi na yenye joto na huepekunane na hatari za kumlisha na maziwa yaliyotengezwa inayokuja kama poda na huchanganywa na maji kisha kutolewa kwa kutumia chupa.

  • Unaeza kupendekeza vyanzo vya hatari kwa mtoto mchanga kutokana na maziwa yaliyotengenzwa vibaya.

  • Kuna hatari ya kuambukizwa kutokana na utengenezaji wa maziwa kwa kutumia maji yaliyochafuliuwa, au ikiwa chupa na chuchu hazitasafishwa kabisa. Ikiwa mama atamlisha mara kwa wakati mmoja, na hawezi kuhifadhi katika sehemu baridi kwa sababu hakuna vifaa vya kuhifadhia katika sehemu baridi, bakteria inamea katika maziwa yenye joto. Vile vile, ikiwa ataweka poda nyingi au kidogo sana katika kila chupa, mtoto atashikwa na utapiamlo ikiwa kemikali ni hafifu sana au kupata kiwango kikubwa sana katika ogani zake kutokana na ukolezi mwingi wa kemikali.

    Mwisho wa jibu

Maziwa ya titi huwa na elemeti zinazopigana na maambukizi, kama vile kingamwili, seli hai na molekuli zinazosaidia mwili wa mtoto kupigana na maambukizi. Pia inahimiza ukuaji wa bakteria yenye faida katika utumbo wa mazwa. Vitu hivi vya maziwa ya titi husaidia kuzuia magonjwa ya kuhara, visababishi vikuu vya vifo vya wachanga kutoka jamii masikini.

Maziwa ya mama pia hupunguza hatari ya aleji kwa mtoto mchanga. Aleji ndio hupinga mabadiliko ya mwili dhidi ya elemeti za lishe, chavua kutoka kwa mimea, wanyama na vitu vingine visivyokuwa na athari vinavyoguza mwili au zinazoingia ndani kupitia pua, kinywa au macho. Watoto wako katika hatari zaidi ya aleji ikiwa kuna historia nzito ya aleji ya familia.

7.2 Ni nini manufaa ya unyonyeshaji?

7.2.2 Manufaa ya unyonyeshaji kwa mama