7.2.2 Manufaa ya unyonyeshaji kwa mama

Unyonyeshaji ni (karibu) bure – mama anahitaji chakula cha kuongezea wakati ananyonyesha, lakini bei ni angalau rahisi kuliko kunua lishe ya fomula/kemikali, chupa na chuchu. Kila wakati hupatikana mara moja, kwa hivyo mama hanashida ya kusafisha kabisa chupa na chuchcu, na kutengeneza lishe za kemilaki mara nyingi kila siku. Inatosheleza kihisia kwa mama kunyonyesha mtoto vizuri na uhusiano husaidia kuleta uelewano bora kati yao.

Homoni (oksitosini) ndiyo hufanya maziwa kububujika kutoka kwa matiti kwa kupunguza misuli ndogo zilizokaribu na chuchu vile vile zilizokaribu na uterasi. Kwa hivyo unyonyeshaji unasaidia uterasi kurudia hali yake ya kawaida.

  • Ni manufaa gani mengine ambayo unaweza kupendekeza yanayotokana na upunguaji wa miometriumu (safu ya msuli ulio katika uterasi)

  • Upunguaji husaidia kufunga mishipa ya damu iliyoraruka mahali plasenta umeshikana na ukuta wa uterasi na hii hupunguza kiasi cha uvujaji wa damu katika uke wakati wa kipindi cha kuzaa/puperiumu na kupunguza hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa.

    Mwisho wa jibu

Unyonyeshaji husaidia mama kupoteza uzani wa ziada alizoongeza wakati wa ujauzito. Ujauzito ndio hubadilisha maumbo ya matiti ya mwanamke bali sio unyonyeshaji.

7.2.1 Manufaa ya unyonyeshaji kwa mtoto mchanga

7.2.3 Unyonyeshaji na kudhibiti muda wa kuzaliwa