7.2.3 Unyonyeshaji na kudhibiti muda wa kuzaliwa
Unyonyeshaji wa kipekee kwa watoto walio na umri wa chini ya miezi sita (kulisha mtoto kwa kutumia maziwa ya mama bila viowevu au vyakula vingine) hupunguza sana nafasi ya mama kuwa mjamzito tena iwapo itaanzishwa mwanzoni (katikati ya saa moja ya kuzaa), na kudumishwa kwa miezi sita ya kwanza iliyopendekezwa. Waeleze mama na mpenzi wake kwamba ikiwa mwanamke anajishirikisha na ngono na hafanyi unyonyeshaji wa kipekee kwa watoto walio na umri wa chini ya miezi sita, anaweza kuwa mjamzito haraka wiki nne baada ya kuzaa. Hivyo basi, taarifa juu ya wakati wa kuanza njia za kupanga uzazi zitatofautiana ikiwa mwanamke ana nyonyesha au la.
Katika Afrika inapendekezwa kwamba ujaribu kuwashawishi kina mama kuwapatia watoto unyonyeshaji wa kipekee kwa miezi sita kwa sababu nyingi, ikiwa ni pamoja na kukandamiza mzunguko wake wa hedhi, lakini tu ikiwa atatimiza vigezo vifuatavyo:
- Mtoto anapaswa kunyonyeshwa kwa kipekee akihitaji akiwa na umri wa chini ya miezi sita (wakati wowote mtoto anataka kulishwa) kati ya kiwango cha chini ya mara 8 hadi12 kwa siku, ikiwa ni pamoja na angalau lishe moja usiku.
- Muda baina ya lishe ya mchana haipaswi kuwa zaidi ya masaa manne na lishe ya usiku haipaswi kuwa zaidi ya masaa sita.
- Kama vipindi vyake vya hedhi vitarudi sawa wakati wa kunyonyesha kwa mtoto aliye na umri wa chini ya miezi sita, anaweza kupata mimba kwa urahisi!
Sisitiza kwamba baada ya miezi sita, hatakuwa salama kutokana na kuwa mjamzito kwa kunyonyesha pekee. Anapaswa kuchagua upangaji mwingine wa uzazi. Utajifunza yote kuhusu haya katika Moduli kuhusu upangaji wa uzazi katika mtaala huu. Jedwali 7.1 linatoa muhtasari wa manufaa ya unyonyeshaji wa kipekee kwa mama na mtoto mchanga.
Mama | Mtoto mchanga |
---|---|
Ni rahisi sana kuliko ile ya kutengenezwa | Ina lishe kamilifu |
Inapatikana kila mara (tayari) | Ina meng’enywa na kufyonzwa kwa urahisi |
Huridhisha akili | Ni safi na ina joto |
Kupunguka kwa uvunjaji wa damu | Ina dutu za kupambana na maambukizi |
Inaweza kutumika kama udhibiti wa uzazi | Huzuia ugonjwa wa kuhara |
Husaidia kupunguza uzito mwingi mwilini | Hupunguza hatari ya aleji |
Huongeza ari ya kuwaunganisha pamoja na mtoto mchanga | Huongeza ari ya kuwaunganisha pamoja na mama |
7.2.2 Manufaa ya unyonyeshaji kwa mama