7.4 Kumpatia mtoto mchanga joto

Watoto wachanga hushikwa na baridi au joto haraka kuliko watoto wengine au watu wazima kwa sababu hawawezi kudhibiti kwa urahisi halijoto mwilini mwao. Kwa hakika hupatwa na hipothemia, kwa hivyo inamaanisha baridi nyingi kwa mtoto, wakati halijoto katika kwapa au rektamu. Iwapo halijoto ya chini itaendelea kwa muda mfupi, itafanya mfumo wa mwili kukosa kufanya kazi vizuri na hii ni tishio kwa maisha. Hipothemia ni kisababishi kuu cha magonjwa na vifo katika watoto wachanga, haswa watoto wanaozaliwa mapema (Kuzaliwa kabla ya wiki 36 ya ujauzito) na wale wanaozaliwa na uzito wa chini (chini ya gramu 2,500). Kipindi cha 8 cha Somo itakufunza kuhusu matatizo na utunzi wa watoto hawa wadogo au wanaozaliwa mapema.

Kwa kawaida hipothemia husababishwa zaidi na mama kukosa maarifa bali sio nguo za kumpa mtoto joto. Kwa hivyo hakikisha umemwelezea mama umuhimu wa kumweka mtoto katika hali ya joto kila wakati ili kuhakikisha halijoto ya kawaida ya mwili imedhibitiwa, juu ya sentigredi 36.5 na chini ya 37.5.

7.3.3 Upunguzaji wa hatari ya virusi kutokana na unyonyeshaji

7.4.1 Jinsi ya kupima halijoto ya mtoto mchanga.