7.4.2 Je, ni wakati gani watoto wachanga wako katika hatari kubwa ya kupata hipothemia?

Watoto wachanga wanalio na matatizo hasa ya kutengeneza joto ya kutosha katika miili yao, au ambao hupoteza joto jingi kwa sababu ya matunzo mabaya kutoka kwa mama, wamo hatarini zaidi.

Watoto wachanga ambao wanaweza kukosa kutengeneza joto la kutosha ni pamoja na wale ambao:

  • Hawajatimiza umri wa kuzaliwa
  • Wana uzito wa chini wakati wa ukilinganisha na umri wa ujauzito.
  • dhoofika (konda)
  • Walioambukizwa
  • Hypoxic (upungufu wa oksijeni wakati wa uchungu wa kuzaa na wanapozaliwa).

Watoto wachanga wanaopoteza joto kupita kiasi ni pamoja na wale ambao:

  • Ulowa baada ya kuoshwa, au kuachwa na nguo zilizolowa
  • Hawajalishwa ya kutosha
  • Wameachwa kwa mazingira baridi, bila mavazi au mapambo ya kutosha, hasa wakati wanapolala
  • Huwa uchi wakati wana nyonyeshwa
  • Hulishwa karibu na dirisha baridi, katika upepo baridi.

7.4.1 Jinsi ya kupima halijoto ya mtoto mchanga.

7.4.3 Ni jinsi gani watoto wachanga hupoteza joto?