Malengo ya Somo la Kipindi cha 8
Baada ya somo hili, unatarajiwa:
8.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandikwa kwa herufi nzito. (Swali la Kujitathmini 8.2 )
8.2 Kueleza ni kwa nini watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini wanahitaji utunzaji maalum, kisha uorodheshe matatizo yanayoweza kuwakumba mara nyingi. (Swali la Kujitathmini 8.1 )
8.3 Kutoa uainisho wa watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula kwa kurejelea umri wa ujauzito na uzani wa wakati wa kuzaliwa, na ueleze mikakati mwafaka ya kudhibiti hali hizi katika kila kauli. (Swali la Kujitathmini 8.2 )
8.4 Kueleza jinsi unavyoweza kumshauri mama kuhusu jinsi ya kumlisha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula au akiwa na uzani wa chini. (Swali la Kujitathmini 8.3 )
8.5 Kueleza jinsi ya kuwakinga watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini kutokana ha hipothemia, ukijumuisha kumshauri mama na familia yake kuhusu Utunzaji wa Mama wa aina ya Kangaruu. (Swali la Kujitathmini 8.4 )
Kipindi cha 8 Utunzaji Maalum kwa Watoto Waliozaliwa Kabla ya Kuhitimu Muhula na Waliozaliwa wakiwa na Uzani wa Chini
