8.1 Je, ni kwa nini watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini wanahitaji utunzaji maalum?

Watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini wako katika hatari zaidi ya kufa kutokana na hipothemia, maambukizi, matatizo ya kupumua na kutokomaa kwa viungo muhimu. Kinachofuatia ni kuwa watoto hawa hushindwa kukabiliana na maisha nje ya uterasi. Sababu kuu zinazowafanya wahitaji utunzaji maalum zimeandikwa kwa muhtasari katika Jedwali 8.1

Kisanduku 8.1 Sifa bainifu za watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa nauzani wa chini

  • Baadhi ya sehemu za mfumo wao wa neva hazijakua vyema.
  • Watoto hawa wana kiwango kidogo cha mafuta ya ngozi, hasa mafuta ya rangi ya kahawia. Mafuta haya ni muhimu sana katika kutolesha joto kwa mtoto mzawa. Mafuta haya hupatikana mabegani, mgongoni, shingoni, kwapani na figoni.
  • Watoto hawa hawachezi, hivyo hawatoleshi joto, ambalo hutoleshwa kwa kucheza sana.
  • Watoto hawa wana uwiano mkubwa wa uzani na sehemu ya juu ya mwili ikilinganishwa na ule wa mtoto mkubwa au mtu mzima. Kwa hivyo, watoto hawa hupoteza joto kwa haraka kupitia ngozini.
  • Watoto hawa wana mapafu ambayo hayajakomaa, hivyo wana matatizo ya kupumua.
  • Watoto hawa hawana kingamwili imara, hivyo wako katika hatari kuu zaidi ya kuambukizwa.
  • Vena za ubongo wao ni nyembamba na hazijapevuka hivyo zinaweza kuvuja damu kwa urahisi.
  • Watoto hawa wanaweza kuwa dhaifu sana hata wasile vyema.

Mfano mmoja wa sababu inayowafanya watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini kuhitaji utunzaji maalum ni kuwa wana uwezo mdogo kupindukia wa kukabiliana na maradhi ambukizi. Hii ni kwa sababu kingamwili yao haijakomaa vyema. Kwa hivyo, kando na linalohitajika kwa watoto wote, wewe na mama mnafaa kuwa waangalifu kuhusu usafi na hatua za kuzuia maambukizi (kama ilivyoelezwa katika Kipindi cha 6). Yeyote anayemshika mtoto anafaa kwanza anawe mikono vyema kabisa, kisha amshike kwa uangalifu. Ngozi ya mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula au akiwa na uzani wa chini inaweza kuchibuka kwa urahisi, hivyo kusababisha maambukizi kuingilia mle.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 8

8.2 Uainishaji wa sifa bainifu za watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini