8.2.2. Uainishaji kwa kuzingatia umri wa ujauzito
Mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula ni aliyezaliwa kabla ya wiki 37 za ujauzito kuisha. Kwa kuzingatia umri wa ujauzito, watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula wameainishwa zaidi kama ifuatavyo:
Mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula: Watoto waliozaliwa katika umri wa ujauzito wa wiki 32 - 36, kama ilivyokokotolewa kutokana na tarehe ya mwisho ya kipindi cha hedhi ya mama. Watoto hawa wanaweza kuhudumiwa vyema nyumbani kwa kuzingatia utunzaji na usaidizi zaidi. Utajifunza kuhusu haya baadaye katika Kipindi hiki.
Mtoto aliyezaliwa siku nyingi kabla ya kuhitimu muhula: Watoto waliozaliwa katika umri wa ujauzito wa wiki 28-31, kama ilivyokokotolewa kutokana na tarehe ya mwisho ya kipindi cha hedhi ya mama. Watoto hawa wana matatizo ya kula na kudhibiti kiwangojoto cha mwili wao kama watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula, na kwa sababu sawa na zao. Ikiwezekana, wanafaa kupewa rufaa mara moja ili kupewa utunzaji maalum hospitalini.
Jedwali 8.1 inaainisha kwa muhtasari yale ambayo tumeeleza, pamoja na hatua unazo hitaji kuchukua.
Uzani wa wakati wa kuzaliwa na umri wa ujauzito | Uainishaji | Hatua |
---|---|---|
Uzani wa chini ya gramu 1,500. | Uzani wa chini sana wa wakati wa kuzaliwa | Mpe rufaa ya DHARURA hadi hospitalini, na uhakikishe amepashwa joto wakati wa kusafiri |
Umri wa ujauzito wa chini ya wiki 32 | Mtoto aliyezaliwa siku nyingi kabla ya kuhitimu muhula: | Hakikisha mtoto huyu amepashwa joto na umpe rufaa mara moja. |
Uzani wa gramu 1,500 - 2,500. | Uzani wa chini wa wakati wa kuzaliwa | Iwapo hakuna tatizo lingine, mshauri mama kuhusu kunyonyesha mwafaka, kuzuia maambukizi na kumpasha mtoto joto. |
Umri wa ujauzito wa wiki 32- 36 | Mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula | Ni kama ilivyoelezwa kuhusu mtoto aliyezaliwa na uzani wa chini wa wakati wa kuzaliwa |
Uzani ulio sawa na au zaidi ya gramu 2,500 na umri wa ujauzito ulio sawa na au zaidi ya wiki 37 | Uzani wa kawaida na kipindi cha kuzaliwa kilichokamilika | Ni kama ilivyoelezwa kuhusu mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula na akiwa na uzani wa chini wa wakati wa kuzaliwa. |
8.2.1 Uainishaji kwa kuzingatia uzani wa wakati wa kuzaliwa