8.3.1 Kunyonyesha na kunywesha kwa kikombe

Katika wiki ya kwanza ya maisha ya mtoto, mama anahitaji usaidizi wako na wa familia yake. Hii ni ili kumhimiza aanze kumnyonyesha mtoto bila kumpa vyakula vingine na kuendelea kunyonyesha hadi mtoto wake aliye mdogo kupindukia aweze kunyonya bila tatizo. Watoto wanaozaliwa katika wiki ya 34 - 36 ya ujauzito wanaweza kunyonya vyema, lakini wale waliozaliwa siku nyingi kabla ya kuhitimu muhula wanaweza kukumbwa na tatizo la kunyonya. Kumnyonyesha mtoto aliyezaliwa mapema sana kabla ya kuhitimu muhulanhuwa changamoto. Mtoto huyu anafaa kunyonya kila baada ya saa 2, ikiwa ni pamoja na usiku.

Iwapo watoto waliozaliwa kabla ya wiki 34 hawawezi kunyonya vyema, wanaweza kupewa maziwa yaliyokamuliwa, kwa kutumia kikombe safi kabisa. (Tutaeleza jinsi ya kufanya hivi katika kifungu kijacho.) Watoto wadogo kwa kimo au waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula ambao wanaweza kunyonya pia wanaweza kuhitaji kupewa maziwa kwa kikombe ili kuhakikisha kuwa wanapata lishe la kutosha. Watoto wote wanaopewa maziwa kwa kikombe wanafaa kupewa takriban ml/kilo 60 kwa siku (yaani mililita 60 kwa kila kilo ya uzani wa mtoto kila siku). Kiwango hiki kinafaa kuongezwa kwa ml/kilo 20 jinsi mtoto anavyohitaji kulishwa zaidi.

Watoto waliozaliwa baada ya wiki 32 za ujauzito huenda wasiweze kunyonya hata kidogo, hivyo wanahitaji kuanzishiwa kupewa vinywaji vinavyotiwa kwa mipira. Hii ni sababu mojawapo wa zinazosababisha mtoto aliyezaliwa kabla ya wiki 32 za ujauzito anafaa kupelekwa rufaa hadi katika kituo cha afya mara moja.

8.3 Ushauri kuhusu jinsi ya kuwalisha watoto waliozaliwa kabla ya wakati na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini

8.3.2 Vidokezo vya kumsaidia mama kumnyonyesha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula au aliyezaliwa akiwa na uzani wa chini.