8.3.3 Kukamua maziwa ya titi la mama

Inaweza kumchukua mama dakika 20-30 kukamua maziwa ya titi, au hata muda zaidi mwanzoni, lakini mama huongeza kasi ya kukamua pindi anavyopata uzoefu. Kwanza mshauri mama anawe mikono na kuosha matiti kwa sabuni na maji, kisha aikaushe kwa taulo taulo safi kabisa. Kiandae kikombe safi kilichochemshwa au chupa iliyo na mdomo mkubwa. Iwapo hawezi kuchemsha kikombe chote, kitie maji yanayochemka na uyaache mle hadi muda mchache kabla ya kutia maziwa. Kisha yamwage yale maji. Maziwa hukingwa dhidi ya bakteria kwa kufanya hivi.

Mama anafaa kuketi vyema kisha aegemee kikombe. Mwonyeshe jinsi ya kushika titi kwa ‘mshiko wa C’ (mkono wake ukichukua umbo la C kubwa; Kielelezo 8.2a). Finya nyuma kidole gumba na vidole vingine kuelekea kifuani (Kielelezo 8.1b), kisha ukizungushe kidole gumba kwenda mbele kana kwamba unatolesha alama za kidole. Hii ni ili kuyatoa maziwa kutoka sehemu zote za titi. Kamua titi moja kwa angalau dakika 3 - 4 hadi maziwa yapungue, kisha ukamue hilo lingine. Kuwaza kuhusu mtoto wake anapokamua kunaweza kufanya maziwa yachuruze kwa urahisi zaidi.

Mchoro 8.2 Kukamua maziwa ya titi (a) Shika titi kwa mshiko wa C; (b) zungusha vidole na kidole gumba kwenda nyuma na mbele ili maziwa yachuruze kutoka chuchuni hadi ndani ya kikombe kilichotakaswa.

Maziwa yaliyokamuliwa kisha yakawa baridi au yaliyowekwa kwa saa 6 yanafaa kutupwa

Maziwa ya titi yanaweza kuhifadhiwa katika kiwango joto cha chumbani kwa saa 6 iwapo chumba hicho hakina joto jingi, na maziwa yamehifadhiwa ndani ya kifaa kilichotakaswa. Hata hivyo, maziwa haya yanaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu zaidi ndani ya friji, iwapo mama anayo. Popote yalipohifadhiwa, maziwa yanafaa kupashwa joto hadi kiwango cha joto la mwili kabla ya kumpa mtoto. Kitie ndani ya bakuli yenye maji moto kifaa kilicho na maziwa yaliyohifadhiwa ili kuyapasha joto. Usichemshe maziwa ya matiti ya mama! Virutubishi na antibodi za maziwa ya mama huharibiwa yanapochemshwa.

8.3.2 Vidokezo vya kumsaidia mama kumnyonyesha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula au aliyezaliwa akiwa na uzani wa chini.

8.3.4 Mwonyeshe mama jinsi ya kumnywesha mtoto kwa kikombe