8.3.4 Mwonyeshe mama jinsi ya kumnywesha mtoto kwa kikombe

Mchoro 8.3 Kumnywesha mtoto aliye mdogo kupindukia huhitaji uangalifu na subira.

Mwonyeshe mama na watu wengine wa familia jinsi ya kumshika mtoto kwa karibu huku wakiwa wameketi wima. Shikilia kwenye mdomo wa chini wa mtoto kijikombe safi sana cha maziwa ya mama yaliyokamuliwa. Mtoto anapoamka na kufungua kinywa, shikilia kikombe midomoni mwake ukimwacha anywe kwa utaratibu. Mpe mtoto wakati wa kumeza na kupumzika kila baada ya kupiga funda. Mtoto anapokunywa vya kutosha na kukataa kunywa zaidi, muweke begani kisha umfanye apige mbweu kwa kumsugua mgongoni taratibu ili kuitoa hewa ambayo huenda aliimeza pamoja na maziwa.

  • Je, ni vidokezo na mitindo gani ya kunyonyesha unayofaa kumweleza au kumfunza mama aliyezaa kabla ya kuhitimu muhula?

  • Unafaa kumwarifu kuhusu:

    • Umuhimu wa kunywesha mtoto kwa maziwa yake kila wakati.
    • Kukamulia matone machache ya maziwa midomoni mwake ili kumshawishi kuanza kunyonya.
    • Jinsi ya kukamua maziwa yake na kuyahifadhi vyema.
    • Jinsi ya kumnywesha mtoto kwa kikombe

    Mwisho wa jibu

8.3.3 Kukamua maziwa ya titi la mama

8.4 Utunzaji maalum ili kuhakikisha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula na aliyezaliwa akiwa na uzani wa chini amepashwa joto