8.4 Utunzaji maalum ili kuhakikisha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula na aliyezaliwa akiwa na uzani wa chini amepashwa joto

Watoto hawa hukumbwa na ugumu wa kudhibiti kiwangojoto cha mwili. Watoto hawa hupoteza jotomwili kwa urahisi, hivyo wapo katika hatari ya kupata hipothemia katika hali hii. Kila mara, fuata kanuni ya ’warm chain’ unapomhudumia mtoto yeyote, bila kuzingatia uzani au umri wake, kama ulivyojifunza katika Kipindi cha 7. Hata hivyo, watoto waliozaliwa muda mrefu kabla ya kuhitimu muhula na walio wadogo sana wanafaa kupewa huduma maalaum ifuatavyo:

  • Punde baada ya kuzaliwa, mlaze mtoto huyo ngozi yake ikiguzana na ya mama, kisha ufuatilishe Utunzaji wa Mama wa aina ya Kangaruu, iliyoelezwa hapa chini.
  • Blanketi au shuka za ziada zilizotengezwa kwa pamba zinahitajika ili kumfunika mama na mtoto. Jambo muhimu la kukumbuka (linalosahaulika mara nyingi) ni kwamba kichwa cha mtoto kinahitaji kufunikwa vyema. Hii ni kwa sababu zaidi ya 90% ya jotomwili hutokea kichwani kisipofunikwa vyema.
  • Chumba anapotunziwa mtoto kinafaa kuwa na kipasha joto cha ziada.
  • Kawisha kumwosha mtoto kwa angalau saa 28 baada ya kuzaliwa, ukitumia maji vuguvugu kila unapomwosha.
  • Anzisha kumnyonyesha mtoto au kumnywesha kwa kikombe muda mfupi iwezekanavyo baada ya kuzaliwa. Mnyweshe mtoto kila baada ya saa 2.
  • Ni jabo gani unalofaa kuzingatia ili kuhakikisha kuwa mtoto amepashwa joto?

  • Unakumbuka kama tulivyo jifunza katika Kipindi cha 7 kuwa ni muhimu kumkinga mtoto kutokana na baridi - hivyo basi, hakikisha kuwa milango na madirisha yote yamefungwa.

    Mwisho wa jibu

8.3.4 Mwonyeshe mama jinsi ya kumnywesha mtoto kwa kikombe

8.5 Utunzaji wa aina ya Kangaruu wa Mama kwa Mtoto