8.5 Utunzaji wa aina ya Kangaruu wa Mama kwa Mtoto

Utunzaji wa aina ya Kangaruu wa Mama kwa Mtoto (UKM) ni njia ya utunzaji iliyopewa jina kwa kurejelea jinsi kangaruu wanavyowatunza ndama wao. Njia hii imetambulika kuwa bora sana katika kuwatunza watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini. Njia hii huhusisha kumshika mtoto huku mwili wake ukiguzana na wa mama mchana na usiku. Mtu mwingine anaweza kuchukua nafasi ya mama iwapo hawezi kumshika namna hii wakati wote.

Utafiti unaonyesha kuwa njia ya UKM inapotumika, husaidia kudhibiti kima cha mdundo wa moyo na kupumua kwa watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini. Njia hii pia husaidia kupunguza maambukizi na kumwezesha mtoto kuongeza uzani ifaavyo. Njia hii humsaidia mama kwa kuzidisha utoleshaji wa maziwa, na pia kufanikisha kunyonyesha bila kutumia vyakula vya ziada.

8.4 Utunzaji maalum ili kuhakikisha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula na aliyezaliwa akiwa na uzani wa chini amepashwa joto

8.5.1 Utaratibu wa UKM