8.5.4 UKM inafaa kufanywa kwa muda gani?

Ikiwa mama na mtoto wanaridhika kutumia njia hii, inafaa kueendelezwa kwa kipindi kirefu kama inavyowezekana au mpaka mtoto ahitimu muhula wa kuzaliwa (wiki 40) ama mpaka mtoto apate uzani wa gramu 2,500. Iwapo mtoto ana uzani unaozidi gramu 1 800 na kiwango chake cha jotomwili ni dhabiti, hana matatizo yoyote ya kupumua na ananyonya vizuri, anaweza kulishwa kupitia UKM kabla ya wiki 40. Mtoto anapotosheka na UKM humdhiirishia mama yake kupitia, kugaagaa, kuchezacheza, kuondoa miguu na mikono yake kutoka kwenye nguo zilizomfunika na kulia hadi afunuliwe.

Hatimaye, ukifuata maagizo haya na kuwasaidia familia zako kutunza watoto wao waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini kama ilivyoelezwa katika Kipindi hiki, ni hakika kuwa utaokoa maisha ya watoto wengi wachanga. Kunalo jambo muhimu kuliko hili?

8.5.3 Kumshauri mama na familia kuhusu umuhimu wa UKM

Muhtasari ya Kipindi cha 8