Muhtasari ya Kipindi cha 8

Katika Kipindi cha 8 umejifunza kuwa:

  1. Watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na wale wenye uzani wa chini wamo katika hatari ya kufa kufuatia maambukizi, matatizo ya kupumua na hipothemia kwa kuwa hawajakomaa.
  2. Punde tu wanapozaliwa ni muhimu kuainisha watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na wale waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini kulingana na umri wao wa ujauzito na uzani wao wa kuzaliwa, na kupendekeza rufaa kwa wale waliozaliwa wakiwa na umri wa ujauzito wa chini mno na wale walio na uzani wa chini sana.
  3. Unaweza kumshauri mama kikamilifu kuhusu namna ya kumnyonyesha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliyezaliwa akiwa na uzani wa chini, ikiwemo kumlisha baada ya kila saa mbili. Unafaa pia kumfunza jinsi ya kujikamua na namna ya kumnywesha mtoto kwa kikombe ikiwa mtoto hawezi kunyonya vyema kwa kuwa hajakomaa.
  4. Unaweza kumfunza mama na familia yake jinsi ya kutoa Utunzaji wa aina ya Kangaroo ya Mama kwa Mtoto (UKM) na kuwaelezea manufaa ya njia hii, ambayo ni pamoja na kuendeleza kunyonyesha, kudhibiti jotomwili la mtoto, kuongeza uzani mapema, kupumua vyema zaidi na upungufu wa kima cha maambukizi.
  5. UKM huendelezwa usiku na mchana hadi mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula anapofikisha umri wa wiki 40 au mtoto aliyezaliwa akiwa na uzani wa chini anapofikisha angalau gramu 1,800. Mama atahitaji usaidizi zaidi ili kukabiliana na changamoto za UMK.

8.5.4 UKM inafaa kufanywa kwa muda gani?

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 8