Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 8

Kwa vile sasa umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili kutathmini jinsi ulivyojifunza.

Swali la Kujitathmini 8.1(linatathmini Malengo ya Somo la 8.2)

Ni viashirio vipi muhimu vinavyoonyeshwa na watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na wale waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini ambavyo hudhiirisha kuwa wanahitaji utunzaji spesheli?

Answer

Vidokezo vikuu vinavyoashiria kuwa watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na wale waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini huhitaji utunzaji spesheli ni:

  • Kutokomaa kwa mfumo wa kingamwili hivyo kuwa katika hatari ya kuambukizwa.
  • Kuwa na hatari ya kupata matatizo ya utendakazi ya mfumo wa neva na mapafu
  • Hatari ya kupata hipothemia, kwa sababu wana kinga ndogo inayotolewa na mafuta ya mwili, na kuna uwiano mkubwawa sehemu juu ya mwili ikilinganishwa na uzani wa mwili na kutoweza kujizalishia joto.
  • Uwezekano wa ugumu wa kunyonya, hivyo ukosefu wa virutubishi, unaweza kusababisha unyonge na hata kudhoofika kwa kingamwili na mwili kukosa joto.
  • Kuwa hatari ya kushika vibaya, kwa mfano kusasbabisha kuharibika kwa ngozi yake dhaifu ambapo husabisha viingizi vya maambukizi.

Mwisho ya jibu

Swali la Kujitathmini 8.2 (linatathmini Malengo ya Somo la 8.1 na 8.3)

Jaza mapengo katika Jedwali 8.2

Jedwali 8.2 Uainishaji wa watoto wazawa kulingana na uzani wa kuzaliwa na umri wa ujauzito, na hatua za kuchukuliwa.
Uzani wa kuzaliwa na umri wa ujauzitoUainishajiHatua za kuchukuliwa
Uzani wa chini ya gramu 1,500
Walizaliwa wakiwa na umri wa ujauzito wa chini mno
Umri wa ujauzito wiki 32-36Ikiwa hukuna tatizo jingine, mshauri kuhusu kunyonyesha kikamilifu, kuzuia maambukizi na kuhakikisha mtoto amepata joto la kutosha.
Uzani wa kawaida na muhula yote ya ujauzito

Answer

Rejelea Kisanduku 8.1 katika Kitengo cha 8.2.1 na ulinganishe na yale uliyoandika katika jedwali 8.2

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 8.3 (linatathmini Malengo ya Somo la 8.4)

Ulimzuru mama aliye na mtoto aliyezaliwa akiwa na uzani wa gramu 2,000 kwa mara ya kwanza saa 12 baada ya kuzaa. Yamkini ana uwezo wa kunyonya, ingawa sio kwa muda mrefu, na mama yake ana wasi wasi kuwa hawezi kupata maziwa ya kutosha. Je utamshauri vipi?

Answer

Kwa kuwa ana uzani wa gramu 2,000 mtoto huyu ana uzani wa chini, lakini anaonekana kuwa na uwezo wa kunyonya. Hata hivyo, ikiwa mama yake anafikiria kuwa mtoto hapati maziwa ya kutosha kwa sababau anachoka haraka akinyonya, unapaswa kumpendekezea ampatie lishe ya ziada ya maziwa ya mama ya kujikamua na kumnywesha kwa kikombe. Kwanza unapaswa umfafanulie jinsi ya kujikamua na namna ya kuhifadhi maziwa (rejelea Kitengo cha 8.3.3 kama huwezi kukumbuka), kisha umwonyeshe jinsi ya kumnywesha mtoto kwa kikombe.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 8.4 (linatathmini Malengo ya Somo la 8.5)

  • a.Ni mambo gani muhimu ambayo haupaswi kumfanyia mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula ili kumkinga dhidi ya hipothemia.
  • b.Utunzaji aina ya Kangaruu wa Mama kwa Mtoto una manufaa gani katika kuzuia hipothemia?

Answer

  • a.Ili kumkinga mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula au aliyezaliwa akiwa na uzani wa chini asipoteze joto, unapaswa kujiepusha:
    • Kumuosha mtoto hadi baada ya angalau saa 48 baada ya kuzaliwa
    • Kumuacha mtoto bila kofia (90% ya joto hupotezwa kupitia kichwa ikiwa kimefunuliwa)
    • Kumuacha mtoto chumbani bila milango au madirisha kufunguliwa
    • Kusahau kuweka kipasha joto cha ziada chumbani ambamo mtoto amelazwa.
    • Kumvua nguo zote ili kubadilisha nepi.
  • b.Manufaa ya UKM ni:
    • Mtoto hushikwa huku mwili wake ukiguzana na wa mama mchana na usiku, jambo ambalo litahakikisha kuwa kiwango cha jotomwili la mtoto kimedibithiwa kikamilivu.
    • Desturi ya kumshika mtoto huku mwili wake ukiguzana na wa mama husitishwa tu kwa sababu maalum (kubadilishia nepi, kumchunguza kama kitovu kinakauka kama kawaida) hivyo basi kupunguza hatari ya kuachwa kwenye chumba kilicho na baridi.
    • Mtoto hunyonya vizuri na kuongeza uzani haraka (hivyo huzalisha mafuta ya mwili yanayomsaidia kupata joto)
    • Manufaa ya UKM ni kuwa huduma hii unaweza kutolewa na mtu mwingine katika familia ikiwa mama ni mgonjwa au anahitaji kupumzika.

Mwisho wa jibu

Muhtasari ya Kipindi cha 8