Nyenzo-rejea 2: Tafakuri ya mama Msekwa kuhusu mkabala wake

Usuli / maarifa ya somo kwa mwalimu

Mwalimu Msekwa pamoja na walimu wenzake kutoka wilayani kwake walikuwa katika kozi ya mafunzo kazini kuhusu dhana ya kujithamini. Kama sehemu ya kozi, walitakiwa kuwa na shajara (kitabu cha kumbukumbu) kwa muda wa siku mbili wakirekodi wakati wote walipowasifu wanafunzi wao na wakati walipowakatisha tamaa au kupuuzia tabia zao.

Walitumia chati kama ioneshwayo hapa chini ambapo waliweka alama ya vema kuonesha nyakati zote walipotenda mojawapo ya haya. Wakati mwingine ilikuwa vigumu kuweka alama hizo wakati wa somo kwa kuwa walikuwa na kazi nyingi, lakini mwalimu Msekwa aliweka chati hiyo katika kitabu chake cha andalio la somo ili aweze kuweka alama hizo wakati alipokuwa na nafasi, au mara tu alipomaliza kufundisha.

SIKU YA 1
Hisabati
Kiingereza
Science
Masomo ya jamii
Uchoraji
Michezo
SIKU YA 2Hisabati
Kiingereza
Science
Masomo ya jamii
Uchoraji
Michezo

Kielelezo: mwfz-mwanafunzi; wanz- wanafunzi

Walipokwenda katika somo lingine waliombwa kuchunguza data na kubaini waliyoyafanya mara nyingi. Waliwakatisha tamaa wanafunzi madarasani? Kama hivyo ndivyo, wanaweza kutafakari kwa nini walifanya hivyo?

Kwa kutumia majadiliano ya vikundi, mwalimu Kimambo aliwashauri wanafunzi wafikirie wangefanya nini ili kuongeza hali ya kuwatia moyo wanafunzi katika madarasa yao.

Data ya mama Msekwa ilionesha kuwa alikuwa akiwakatisha tamaa wanafunzi katika masomo ya sayansi kuliko katika masomo mengine, na hili lilimshangaza. Hili labda lilisababishwa na imani ya welewa wa masomo ya sayansi na kwa kuwa hakuyapenda masomo hayo ya sayansi. Alijihisi kutokuwa na mpangilio mzuri na wasiwasi wakati wanafunzi walipomuuliza maswali.

Alitayarisha orodha ya vitu ambavyo angevifanya ili kusaidia darasa lake na ushirikiano wake na wanafunzi wake:

  1. Kuwa na masomo yaliyotayarishwa vizuri
  2. Alipima usahihi wa maarifa yake ya masomo
  3. Alifikiria maswali ya kuwauliza wanafunzi wake na majibu aliyotarajia kupata.
  4. Alifikiria jinsi ya kukubaliana na majibu yao, kwa mfano:
    • a.‘hilo ni wazo zuri, lakini unaweza kufikiria zaidi kuhusu.....’ halafu uliza swali la kwanza kwa namna tofauti.
    • b.‘sikuwa nimefikiria wazo hilo- tunawezaje kulioanisha na swali langu la kwanza?

Kwa kila swali mwanafunzi anahimizwa kufikiri zaidi na kushiriki zaidi na hawaambiwi kuwa ni wajinga au wamekosea.

Kama hawaelewi wape wanafunzi wangu nafasi ya kuuliza maswali yao wenyewe kuhusu mada. Waruhusu wanafunzi wengine kujibu badala ya mimi mwenyewe.

Baada ya wiki chache, polepole, alianza kujiamini na kugundua kuwa kwa kuwa alikuwa amejitayarisha vizuri zaidi, hakuwa na wasiwasi na hivyo hakupandisha sauti yake. Wanafunzi wake walianza kuyapenda zaidi na zaidi masomo ya sayansi.

Nyenzo-rejea ya 1: Kutafakari juu ya tabia yako/Kujitafakari tabia

Sehemu ya 5: Vitendo vya kuimarisha ustawi wa kiroho