Namba ya moduli 1: Kusoma na Kuandika kwa madhumuni mbalimbali

Sehemu ya 1: Kuhamasisha na kutathmini usomaji na uandishi

Swali Lengwa muhimu: Unawezaje kuhamasisha ujifunzaji kusoma na kuandika na kutathmini maendeleo?

Maneno muhimu: kujua kusoma na kuandika katika hatua za mwanzo; nyimbo; mashairi; chapa za kimazingira; tathmini; kazi ya kikundi; usomaji wa ushirika.

Matokeo ya ujifunzaji

Mwishoni mwa sehemu hii, utakuwa umeweza:

  • kutumia nyimbo na mashairi kufundisha wanafunzi wa kiwango cha mwanzo kusoma;
  • kutumia ‘chapa za kimazingira’ na bidhaa za dukani kufundishia usomaji, uandishi na uchoraji;
  • kutalii njia za kuhamasisha ujifunzaji kwa kutumia kazi ya kikundi;
  • kukuza uwezo wako wa kutathmini ujifunzaji.

Utangulizi

Msomaji na mwandishi mfanisi anatakiwa ajue na aweze kufanya nini? Kama mwalimu, unatakiwa uweze kujibu swali hili ili uweze kuwaongoza wanafunzi wako. Kujifunza kusoma na kuandika kwa ufanisi kunahitaji mazoezi. Hivyo, ni muhimu kutumia mikabala na shughuli mbalimbali ambazo zitawafanya wanafunzi wafurahie. Ni muhimu kutathmini maendeleo ya wanafunzi na kujiuliza mwenyewe kama unakidhi matakwa yao. Sehemu hii inatalii mawazo haya kwani inaangalia ujifunzaji kusoma na kuandika katika hatua za awali.