Somo la 3

Ili kukubalika kuwa raia wa nchi yoyote unapaswa kuwa umekamilisha vigezo fulani. Vigezo hivi huandikwa katika katiba ya nchi. Jaribu kupata katiba ya nchi yako na zingatia inataja vigezo gani. Nyenzo-rejea 3: Nukuu kutoka katika Katiba inaorodhesha sifa za kuwa raia.

Njia mojawapo ya kutambua maoni ya wanafunzi wako kuhusu uraia imetolewa katika Uchunguzi Kifani 3.

Mabaraza ya shule yanaweza kuhitimisha mjadala kama njia mojawapo ya kuhamasisha wanafunzi. Namna ya kutayarisha baraza imeelezwa katika Shughuli muhimu.

Uchunguzi kifani ya 3: Ugeni wa kiongozi wa serikali za mitaa shuleni kujadili uraia

Mwalimu Notuka wa shule ndogo ya kijijini katika Tanzania, alimkaribisha Afisa wa Wilaya kutembelea darasa lake la tano lenye wanafunzi 56. Afisa huyo alileta picha ya rais, bendera ya taifa, nembo ya taifa, kitambulisho chake cha kazi na pasi ya kusafiria. Aliwaelezea wanafunzi umuhimu wa vitu hivi kwa Mtanzania. Alifafanua kila sehemu ya bendera inamaanisha nini. Waliimba pia wimbo wa taifa na kuorodhesha matukio yote ambayo wimbo huo huimbwa.

Baada ya ugeni huo, Mwalimu Natuko aliwapanga wanafunzi katika makundi madogo yanayozunguka madawati yao na kuwataka wajadili kwa nini ni muhimu kwao kuwa raia wa Tanzania. Alipitapita darasani na kuwaongoza wanafunzi wasijadili nje ya mada na kuorodhesha maoni ya kila mmoja.

Kisha aliwataka kila mmoja aandike maoni yake pekee katika vitabu vyao. Alikusanya kazi zao na aliweza kutathmini kila mmoja amejifunza nini kuhusu uraia.

Kuna wanafunzi watano ambao sababu zao hazikuendelezwa vizuri na Mwalimu Natuko alijadili sababu na wanafunzi hawa wakati wa mapumziko ili kuona kama wameelewa maoni hayo.

Shughuli muhimu: Kuwasilisha ujifunzaji katika baraza la shule

Zungumza na mwalimu mkuu kama unaweza kuwa na mkutano na baraza la shule kuhusu ‘Kuwa raia mwema’

Pamoja na darasa lako jadili maudhui ya baraza yatakuwa yapi

Kila kikundi kinatayarisha sehemu yake na nyenzo zitakiwazo. Itafaa uwashauri wanafunzi wako kuwa yafuatayo yanahitaji kuzingatiwa:

Raia ni nani?

Haki na wajibu nyumbani

Haki na wajibu katika jamii

Ishara za utaifa - bendera, wimbo wa taifa, kitambulisho, nembo, pasi ya kusafiria.

Kwa nini ni muhimu kuwa raia mwema?

Toa kazi mbalimbali na wape nafasi ya kujitayarisha - labda baada ya masomo kadhaa.

Ifanye kazi hiyo wazi, ili kila mwanafunzi aweze kutoa matokeo ambayo unaweza kuyatumia kutathmini ujifunzaji wao.

Wahamasishe waandike mashairi au aya za kusoma, kuchora bendera au tafuta aya ambayo wanapenda kusoma au kutumia.

Kubaliana na mtiririko wa uwasilishaji na fanya mazoezi.

Wasilisha baraza lako katika shule nzima

Baada ya hapo, jadiliana na wanafunzi yapi yamefanyika vizuri na yapi yangefanywa vizuri zaidi. Wana mawazo gani kuhusu jinsi shule nzima ilivyoelewa uraia –vizuri au vibaya?

Nyenzo-rejea ya 1: Haki na wajibu wa watoto- Orodha ya darasa ya mwalimu Nqwinda