Nyenzo-rejea ya 2: Haki za mtoto katika Tanzania

Nyenzo-rejea ya Mwalimu ya kutumia katika kupanga au kurekebisha pamoja na wanafunzi

Kwa kuzingatia mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za mtoto ulioridhiwa mwaka 1991, haki za mtoto ni :

Mtoto katika Tanzania:

Anapaswa kuwa na haki sawa kama mtu mzima, bila kujali jinsia yake, dini, mila, kutoka vijijini au mijijini, uraia, kabila, jamii, hali ya ndoa ya wazazi wake au maoni.

Haki ya kukulia katika mazingira salama, uangalizi mzuri na mazingira salama, na kuwa na mahitaji ya msingi ya maisha, ikiwa ni pamoja na chakula, huduma za afya, mavazi na malazi.

Kuwa na jina na uraia.

Haki ya kujua wazazi wake ni nani na kufurahia maisha kuwa pamoja na familia au familia kubwa zaidi. Mahali ambapo mtoto hana familia au ameshindwa kuishi nao, basi anapaswa kupewa mbadala wa matunzo unaopatikana.

Haki ya kupewa kipaumbele katika mambo anayotaka katika uamuzi wowote uaofanywa kumhusu.

Haki ya kutoa maoni na kusikilizwa, na kushauriwa kwa kuzingatia welewa wake katika maamuzi ambayo yanamuathiri.

Haki ya kupata kinga ya afya yake kwa kupata chanjo na huduma nyingine za kiafya, na kufundishwa jinsi ya kujikinga dhidi ya magonjwa. Anapokuwa mgonjwa, motto anapaswa kutibiwa kikamilifu.

Mtoto mlemavu ana haki ya kushughulikiwa kwa heshima kama watoto wengine na kupewa matunzo maalum, elimu na mafunzo panapohitajika ili kukuza kipaji chake na kujitegemea.

Haki ya kukataa kulazimishwa kuingizwa katika makundi ya kijamii na utamaduni ambayo yanaleta madhara (jando na unyago) ya kiafya.

Haki ya kutendewa kwa haki na kibinadamu katika mfumo wa sheria

Haki ya kulindwa dhidi ya aina zote za unyanyaswaji na unyonywaji.

Haki ya kupata elimu ya msingi.

Haki ya kupata burudani isiyo na madhara kimaadili; kushiriki katika michezo na shughuli za utamaduni chanya na sanaa.

Haki ya kutoajiriwa au kushiriki katika shughuli ambazo zinahatarisha maendeleo ya afya, elimu, akili, mwili na maadili

Mtoto, akiwa katika hali ya dharura ya kivita, mkimbizi au katika hali yoyote ya hatari, basi ana haki ya kuwa kati ya watu wa kwanza kuokolewa na kutunzwa.

Nyenzo-rejea ya 1: Haki na wajibu wa watoto- Orodha ya darasa ya mwalimu Nqwinda

Nyenzo-rejea 3: Nukuu kutoka katika Katiba: Sheria ya uraia ya ikionesha baadhi ya vigezo kwa wale ambao wana sifa za kuwa raia wa Tanzania.