Nyenzo-rejea 3: Nukuu kutoka katika Katiba: Sheria ya uraia ya ikionesha baadhi ya vigezo kwa wale ambao wana sifa za kuwa raia wa Tanzania.

Nyenzo-rejea ya Mwalimu ya kutumia katika kupanga au kurekebisha pamoja na wanafunzi

SEHEMU YA II KUPATA URAIA SIKU YA AU KABLA YA SIKU YA MUUNGANO

4. Raia wa Tanzania bara na Zanzibar kabla ya siku ya Muungano anachukuliwa kuwa amekuwa raia wa Tanzania siku ya Muungano.

  1. Kila mtu ambaye, baada ya kuzaliwa Tanzania bara au Zanzibar kabla ya siku ya Muungano, alikuwa mara moja kabla ya siku ya Muungano raia wa Jamhuri ya Tanganyika au wa Jamhuri ya watu wa Zanzibar atachukuliwa kuwa amekuwa, siku ya Muungano, na, kuanzia siku ya Muungano, kwa kuzingatia kifungu cha 30, kuwa ameendelea, na baada ya kuanza kwa sheria hii ataendelea, kuwa raia kwa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano

  2. Kila mtu, aliyezaliwa nje ya ama Tanzania bara au Zanzibar kabla ya siku ya Muungano, alikuwa mara moja kabla ya siku ya Muungano raia kwa kujiandikisha au kwa kuasiliwa na Jamhuri ya Tanganyika au wa Jamhuri ya watu wa Zanzibar atachukuliwa kuwa amekuwa, siku ya Muungano, na, kuanzia siku ya Muungano, kwa kuzingatia kifungu cha 30, kuwa ameendelea,kuwa raia kwa kujiandikisha au vinginevyo, kwa kuasiliwa na Jamhuri ya Muungano, na baada ya kuanza kwa sheria hii ataendelea, kuwa raia kwa kuzaliwa, kwa kuasiliwa na Jamhuri ya Muungano, na baada ya kuanza kwa sheria hii atakuwa na ataendelea kuwa raia wa kuasiliwa wa Jamhuri ya Muungano.

  3. Kila mtu, aliyezaliwa nje ya ama Tanzania bara au Zanzibar kabla ya siku ya Muungano, alikuwa mara moja kabla ya siku ya Muungano raia kwa ukoo wa Jamhuri ya Tanganyika au wa Jamhuri ya watu wa Zanzibar atachukuliwa kuwa amekuwa, siku ya Muungano, na, kuanzia siku ya Muungano, kwa kuzingatia kifungu cha 30, kuwa ameendelea kuwa raia kwa ukoo wa Jamhuri ya Muungano.

5. Watu waliozaliwa katika Jamhuri ya Muungano siku ya au baada ya siku ya Muungano

  1. Kwa kuzingatia sharti la kifungu kidogo cha (2), kila mtu aliyezaliwa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya au baada ya siku ya Muungano atachukuliwa kuwa amekuwa na kuendelea kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano kuanzia siku ya kuzaliwa kwake, na kuanzia siku ya kuanzishwa kwa sheria hii atakuwa na kuendelea kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano, kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 30.

  2. Mtu hatachukuliwa ni raia au kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa kifungu hiki kama wakati wa kuzaliwa kwake -

    • a.wazazi wake wote hawakuwa raia wa Jamhuri ya Muungano na baba yake, aliyeteuliwa kuwa mwakilishi, ana kinga ya madai na mchakato wa kisheria, ambayo hutolewa kwa mjumbe wa mamlaka ya nchi za nje, katika Jamhuri ya Muungano, au
    • b.mmojawapo wa wazazi wake ni adui na uzazi umetokea katika sehemu ambayo ilikuwa chini ya miliki ya adui.

6. Watu waliozaliwa nje ya Jamhuri ya Muungano siku ya au baada ya siku ya Muungano

  1. Kila mtu aliyezaliwa nje ya Jamhuri ya Muungano siku ya au baada ya siku ya Muungano atachukuliwa kuwa, kuanzia tarehe yake ya kuzaliwa, atachukuliwa kuwa na kuendelea kuwa, kwa kuzingatia mwanzo wa sheria hii atakuwa na kuendelea kuwa, raia wa Jamhuri ya Muungano ikiwa tarehe hiyo ya kuzaliwa kwake baba yake au mama yake ni au alikuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania vinginevyo licha ya ukoo, wa kuzingatia sharti la kifungu cha 30.

Nyenzo-rejea ya 2: Haki za mtoto katika Tanzania

Sehemu ya 2: Njia za kuchunguza masuala ya kijinsia