Somo la 3

Kuna aina nyingi za tabia ya udhalilishaji na ni wanawake na watoto ambao mara nyingi ndio wahanga. Hii haina maana kwamba wavulana hawawezi kudhalilishwa pia; ni kwamba wasichana na wanawake wameelekea kuwa na majukumu hafifu katika jamii, wakati wanaume wamechukua yenye nguvu na madaraka zaidi.

Kama unataka kuchunguza sehemu hii pamoja na darasa lako, unahitaji kufanya maandalizi kwa uangalifu sana ili uweze kuwasaidia wanafunzi wako kwa vile baadhi ya hoja zinaweza kuwafanya wasijisikie vizuri na kuwasuta. Unaweza pia kukuta kwamba unatoa hadharani baadhi ya matukio ya udhalilishaji, ni lazima ujiandae kuwasaidia wanafunzi wako kwa umakinifu mkubwa wa namna ya kuzungumza na kwa uchaguzi mkubwa wa maneno ya kusema.

Unaweza kujiona hujitoshelezi kuzungumzia mada nyeti kama hii peke yako –hivyo unaweza kufuata mwongozo wa Bibi Umoru katika Uchunguzi-kifani 3 , ambaye alimwambia mtu mmoja toka Asasi isiyo ya Kiserikali ya kijamii kuja na kumsaidia kuendesha mjadala kuhusu udhalilishaji.

Uchunguzi kifani ya 3: Kutumia wataalamu wa kijamii katika kusaidia kujadili masuala nyeti

Kwa muda wa wiki kadhaa, darasa la V la Bibi Teri limekuwa likifanya kazi juu ya mitazamo pogofu kuhusu jinsia na jinsi inavyoweza kuathiri vibaya maendeleo ya msichana darasani na katika maisha. Ilikuwa wakati mgumu kwa Bibi Teri kwa sababu wavulana walijisikia hali ibaki hivyo ilivyokuwa na hawakuona kwamba kulikuwa na haja ya kuibadilisha.

Aliamua kupata msaada wa mtaalamu na akawasiliana na Asasi isiyo ya Kiserikali ya kijamii ambao walikuwa wakifanya kazi ya miradi ya maendeleo vijijini katika mji wao. Alikutana na mwanamke aliyeitwa Amina ambaye alikuwa mtaalamu wa jinsia.

Amina alikuja shuleni na alizungumza na darasa kuhusu udhalilishaji. Wanafunzi walitambua kwamba udhalilishaji unaweza kuwa wa kiakili, na vile vile wa kimwili na kijinsia. Amina alisimulia darasa kuhusu hadithi za vijana ambao wamedhalilishwa na wazazi wao, wanafamilia wengine, na hata watu kutoka katika makundi yao ya kidini. Alizungumza pia kuhusu njia ambazo wanafunzi hawa wamekuwa wakisaidiwa; na asasi ambazo ziko kwa ajili ya kuwasaidia watu. Maelezo yake yaliwafanya baadhi ya wanafunzi kuchukizwa sana kwamba watu wanaweza kuwa na tabia mbaya namna hiyo.

Wakati wa mazungumzo, Bibi Teri aliwaona wasichana wawili wakianza kulia. Baada ya ziara ya Amina, Bibi Teri aliwauliza wale wasichana wawili kama wangependa kwenda kuzungumza na Amina. Walikubali. Aliweka miadi ya Amina kukutana nao.

Katika somo lililofuatia, Bibi Teri aliwaambia wanafunzi wake waandike kuhusu udhalilishaji na waeleze hisia zao kuhusu tabia hiyo. Kutokana na zoezi hili, aliweza kuona ni kwa kiasi gani kila mwanafunzi alielewa, na aliweza kuona jinsi walivyoonesha hisia zao kutokana na hadithi za Amina.

Shughuli muhimu: Kuandaa tukio la shule kuhusu masuala ya kijinsia

Baada ya kuchunguza baadhi ya masuala darasani mwako kuhusiana na jinsia, toa pendekezo kwao kwamba wawaelimishe na wengine hapo shuleni kuhusu kile ambacho wao wamekipata.

Waulize watafanikishaje kazi hii. Wanaweza:

  • kutunga mchezo?

  • kufanya mhadhara?

  • kuandika habari hizi katika kitabu?

  • kuandika shairi?

Unaweza kufanya zaidi ya moja ya shughuli hizi ikiwa una darasa kubwa. Wanafunzi wanaweza kuchagua kikundi gani wajiunge nacho.

Mara watakapoamua nini cha kufanya, waambie wapange wanachotaka kukisema na kuchagua mbinu nzuri ya kukisema. Wakumbushe wawe makini na hadhira yao na wawe waangalifu kuhusu jinsi watakavyowasilisha mawazo yao.

Wape muda wa kuandika rasimu au kufanya mazoezi kuhusu wanachokifanya. Wakimaliza, waruhusu wawasilishe mchezo wao, kitabu, shairi au mhadhara mbele ya darasa, ili waweze kupata maoni faafu ambayo yatawawezesha kufanya marekebisho kabla hawajafanya onesho au uwasilishaji kamili mbele ya shule.

Baada ya tukio, wape wanafunzi wako fursa ya kutathmini athari ya tukio waliloonesha.

Tafakari jinsi utakavyowasaidia wanafunzi wako kuifanya kazi hii.

Nyenzo-rejea ya 1: Masuala ya kijinsia