Nyenzo-rejea 3: Igizo kifani kinyume

Nyenzo-rejea ya Mwalimu ya kutumia katika kupanga au kurekebisha pamoja na wanafunzi

Bibi Mutiu amechelewa

Bwana Mutiu yuko kwenye hekaheka za kusafisha nyumba. Amembeba mtoto mgongoni kwa sababu mtoto haachi kulia. Anna, mwenye umri wa miaka mine, anamvuta Bwana Mutiu miguuni kwa sababu anataka kitu cha kula. Ni dhahiri Bwana Mutiu amechoka, lakini chakula cha jioni kinaiva katika moto mdogo. Anawaita watoto wakubwa nje waende kuongeza kuni. Anasema shida zake huku akiendelea na kazi. Ana wasiwasi kwamba chakula kinaweza kisitoshe mkewe atakaporudi nyumbani kutoka kazini kwenye baraza.

Bibi Mutiu anawasili nyumbani. Amekunywa kidogo na ana hasira kwa sababu chakula cha jioni hakiko tayari na nyumba si safi. Anamfokea Bwana Mutiu na wanakuwa na ugomvi, halafu Bibi Mutiu anampiga Bwana Mutiu na anatokomea nje ya nyumba akisema anakwenda kupata chakula chake cha jioni mahali pengine.

Nyenzo-rejea ya 2: Jinsia – unafikiri nini?

Sehemu ya 3: Kuchunguza kazi na ajira