Nyenzo-rejea 3: Hadithi ya mkulima mchoyo

Nyenzo rejea za mwalimu kwa ajili ya kupanga na kutumia na wanafunzi

Kulikuwa na mkulima mmoja kijana. Alikuwa na mke na watoto wawili na waliishi katika kijiji kidogo. Mkulima alirithi shamba lake kutoka kwa babu yake aliyekuwa mchapakazi na ambaye alimpenda sana. Ingawa alikuwa na huzuni kwa kifo cha babu yake, mkulima aliridhika kwa kuwa mmiliki pekee wa ardhi yote.

Alikuwa ni kijana mchapakazi na aliweza kulitunza shamba vizuri, kama si vizuri zaidi, kuliko babu yake. Alijifunza mengi kutoka kwa babu yake lakini pia alijifunza vema shuleni na alisoma mambo mengi kuhusu njia mbalimbali za kuhifadhi maji na kutunza ardhi, jambo ambalo liliongeza mazao yake. Hata hivyo, hakuwa kama babu yake kwa kuwa hakuwagawia wakulima na wazalishaji wengine pale kijijini mawazo au mazao yake ya ziada.

Wanakijiji walishangaa walipokwenda kumwomba mbegu au ushauri kwa kuambiwa kwamba watoke katika ardhi yake. Mke wake hakupenda tabia hii lakini aliheshimu mawazo ya mumewe. Wanakijiji walitazama alichofanya na baadhi wakajaribu kuiga mambo aliyoyafanya bila kupata mafanikio makubwa. Wengine walicheka au kunung’unika kwa aliyoyafanya.

Wakati mmoja wa msimu wa kiangazi, mazao hayakustawi vizuri katika kijiji kile. Kulikuwa na maji kidogo kwa sababu kijito kilikauka hivyo kulikuwa na mwendo mrefu wa kilometa sita kuelekea kwenye chanzo kingine cha maji. Maana yake ni kwamba maji yaliyoletwa nyumbani yalitumika kwa kunywa tu.

Hata hivyo, mkulima mchoyo, alikuwa na maji na chakula kingi, lakini hakuwasaidia wanakijiji ambao walikuja kuomba msaada. Mkewe alimwomba awasaidie lakini hakubadili msimamo wake. Alitengeneza mifereji na kingo ili kukusanya maji ya mvua na aliyahifadhi katika mapipa makubwa ambayo alikuwa nayo. Kwa hiyo ukame ulipotokea aliweza kumwagilia mimea yake, ambayo ilikua vizuri kama kawaida.

Jinsi kulivyoendelea kuwa na joto na kiangazi kikali, mazao ya watu yalianza kufa na watu wengi wakapatwa na njaa. Mke alijaribu kumshawishi mumewe awasaidie wanakijiji. Watoto walijaribu kumshawishi baba yao, lakini hakuwasikiliza. Alisema alifanya kazi kwa bidii hivyo mazao ni mali yake, na wengine walikuwa wavivu au hawakuangalia yatakayotokea mbele.

Hata hivyo, siku moja, mtu aliyekonda sana na mwenye nguo zilizoraruka alifika shambani kuomba msaada wa chakula kwa ajili ya mke wake ambaye alikuwa mgonjwa. Mkulima alimfukuza kwa ukali lakini mke wake alimzuia na kusema: ‘Humtambui mpwa wako?’ Mkulima alipatwa na mshtuko kwa jinsi mpwa wake alivyoonekana amekonda na amezeeka. Mpwa alielezea jinsi alivyojaribu kutunza maji lakini alishindwa, na jinsi mazao yake yalivyokufa.

Mkulima akamweleza anachotakiwa kufanya wakati mwingine. Lakini mke wake akasema amedhoofika mno kiasi cha kushindwa kufanya hayo, vinginevyo umpe chakula yeye na mke wake. Mkulima alitulia na akampa mpwa wake chakula. Mpwa alirudi wiki iliyofuata akasema mkewe amepata nafuu na kuomba chakula zaidi. Mkulima alitaka kukataa, lakini mkewe akamwambia kwamba walikuwa na njaa sana kwa hiyo haikutosha kuwapa fungu moja tu la chakula. Mkulima aliwapa chakula, na katika kipindi cha siku chache zilizofuata, taratibu alibadilika mawazo yake baada ya kutafakari kuhusu uchoyo na utovu wa busara kuhusiana na kumbukumbu ya babu yake na shida ya majirani zake. Kwa hiyo aliwaita wanakijiji shambani kwake, akawagawia chakula na kuahidi kuwasaidia kujiandaa vizuri kwa ajili ya msimu ujao wa mazao.

Nyenzo-rejea ya 2: Shajara ya matumizi ya maji

Nyenzo-rejea 4: Maswali kuhusu utumizi wa ardhi